Wednesday, May 24, 2017

WAZIRI DK. MWAKYEMBE AONGOZA MAPOKEZI YA SERENGETI BOYS

Timu hiyo ya vijana ilikuwa jijini Libreville nchini Gabon kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika ya vijana iliyofanyika katika miji miwili ya Libreville na Port Gentil ambako iliondolewa kwenye hatua ya makundi na Niger. 

Serengeti Boys ilifungwa bao 1-0 na Niger katika mchezo uliofanyika Port Gentil, hivyo kufanya matokeo ya timu zote mbili yaani Niger na Tanzania kufanana kwa pointi, idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa tangu kuanza kwa fainali hizi za AFCON, Mei 15, mwaka huu.
Serengeti Boys iliyokuwa Kundi B iliondolewa Kundi B iliondolewa na Niger iliyopenya kwenda hatua ya Nusu Fainali kwa faida ya kupata ushindi katika mchezo ambao umekutanisha timu hizo kwani Tanzania ilifungwa 1-0 katika mchezo wa mwisho hatua ya makundi.  

Kanuni hiyo ya mashindano ya CAF inajieleza kuwa matokeo ya ‘head to head’ kwa maana zinapokutana timu mbili zenye uwiano wa pointi na magoli matokeo huamualiwa kwa mshindi kupewa nafsi katika mchezo uliokutanisha timu hizo mbili.

……………………………………………………………………..……………..……
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA



No comments: