Saturday, June 3, 2017

MADRID YA ZIDANE BINGWA WA UEFA 2017

Real Madrid celebrateHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWachezaji wa Real Madrid wakisherehekea kutwaa ubingwa Ulaya, mara yao ya 12 kuibuka mabingwa
Klabu ya Real Madrid ya Uhispania imeicharaza Juventus ya Italia 4-1 na kushinda Kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Mreno Cristiano Ronaldo alifunga mabao mawili, la kwanza kwake na klabu dakika ya 20 na lake la pili dakika ya 64 kutoka kwa krosi ya Luka Modric.
Casemiro aliwafungia Real bao lao la pili dakika ya 61 kabla ya Marco Asensio kukamilisha ushindi wao dakika ya 90 kwa bao lao la nne.

No comments: