Monday, June 12, 2017

Ripoti Maalum mambo yote yaliyojiri uwasilishwaji wa Kamati ya Pili ya Mchanga wa madini

Leo Kamati ya Pili ya Mchanga wa Madini Inawasilisha Ripoti Yake kwa Rais John Pombe Magufuli.
Msikilize hapo chini rais akizungumza baada ya kupokea ripoti hiyo. 


 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli leo Jumatatu June 12 amepokea ripoti ya kamati ya pili ya uchunguzi wa mchanga wa madini.
****
1.Kamati ya wanasheria na wachumi ya kuchunguza mchanga wa madini iliteuliwa Aprili 10 ikiongozwa na Prof. Nehemiah Osoro.

2.Miongoni mwa hadidu za rejea ambazo kamati ilipewa ni kujua idadi ya makotena yaliyosafirishwa nje ya nchi tangu 1998.

3.Kamati pia ilitakiwa kuchunguza kama Tanzania inauwezo wa kutengeneza 'smelter' nchini, gharama zake na muda utakaotumika. 

4.Kamati ilitakiwa kuchunguza tofauti ya mapato ambayo Tanzania ilipata na ambayo ilitakiwa kuyapata tangu mwaka 1998. 

5.ACACIA inayojinasibu kama mmiliki wa migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi haijawahi kuwasilisha nyaraka za umiliki huo.

6. Kamati imebani kwa mujibu wa nyaraka kuwa kampuni ya ACACIA PLC haikusajiliwa nchini 

7.Kamati imebaini kuwa wamiliki wa makampuni ya madini nchini wametenda makosa mbalimbali ya jinai. 

8.Kamati imeridhia baadhi ya watumishi wa serikali, makampuni ya usafirishaji na TMAA wameliingiza Taifa hasara kwa makusud. 

9.Makampuni ya Pangea na Bulyahulu yamepatikana na hatia ya kuliingizia Taifa hasara kwa kutokutoa taarifa sahihi juu ya uzito wa makinikia:. 

9.Idadi na uzito wa makontena ya mchanga ulionekana kuwa mkubwa kwenye meli tofauti na kwenye nyaraka za bandarini. 

10.Baadhi ya makampuni ya wakala wa meli ziliwasilisha nyaraka za uongo za usafirishaji wa madini kati ya 1998 na 2017. 

11.Makontena 30 ya futi 20 yenye makinikia yalionekana kwenye nyaraka yamesafirishwa, lakini ukweli yalisafirishwa 33. 

12.Kupitia hati ya usafirishaji wa makontena melini, idadi kubwa ya makontena yalikuwa yakisafirishwa bila kuorodheshwa. 

13.Migodi ya Bulyanhulu na Pangea imekuwa ikipata faida lakini faida halisi haikuwa ikionyeshwa. 

14.Kamati imebaini makontena 44,277 kwa kiwango cha chini yalisafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 na 2017. 

15.Viwango vya dhahabu kwa kila kontena ni 28kg, kwa miaka yote ni tani 1,240 kwa kiwango cha chini, thamani yake Tsh 108tril 

16.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 ni trilioni 132.56 kwa kiwango cha chini.

17.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 ni trilioni 229.9 kwa kiwango cha juu.

18.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 kwa Kiwango cha wastani ni trilioni 188.58

19.Kodi ya Mapato ambayo Tanzania imepoteza tangu 1998 hadi Machi 2017 ni trilioni 55 katika usafirishaji wa makinikia.

20.Kodi ya Zuio ambayo Tanzania imepoteza tangu 1998 hadi Machi 2017 ni bilioni 94 katika usafirishaji wa makinikia.

21.Mh Rais jumla ya Kodi tulizopoteza ni Sawa na makadirio ya bajeti ya serikali kwa kiwango cha Mwaka 2017/18 kwa miaka 2.

22.Taarifa ambazo zimekuwa sikiwasilishwa TMAA kuhusu uchenjuaji wa makinikia hazina ukweli wowote.

23.Mh Rais kamati imepata mikataba ya mauzo ya uuzwaji Wa makinikia nje ya nchi kuwa serikali haihusiki kabisa.

24.Mikataba hiyo Mh Rais haina Masharti kuwa Serikali inapaswa kupewa taarifa ya uuzwaji wa Makinikia kutoka ktk migodi.

25.Mh Rais katika uchunguzi wetu Serikali ina hisa asilimia 15 ikauza 5 na kila mwaka kamishna au Waziri wa Fedha hupokea dola laki 1.

26.Pangea Gold mine ina mikataba miwili ilisainiwa na Mh Daniel Yona baadaye Mh Nazir Karamagi serikali haina hisa Yoyote.

27.Mh Rais Mkataba wa North Mara ulisainiwa na Waziri Daniel Yona Mwaka 1999 baadaye Nazir Karamagi Mwaka 2017

28.Mh Rais katika Mkataba wa Geita Gold Mine ulisainiwa na Mh Abdallah Kigoda na serikali haina Hisa hata moja.

29.Kamati imebaini kuwa kumekuwa na uongezaji wa muda wa leseni na maeneo uchimbaji kinyume na sheria.

30.Mh Rais kamati imebaini kuwa Mh William Ngeleja na Sospeter Muhongo walitoa mikataba mipya bila kufuata sheria za nchi

31.Mh Rais Mkataba wa North Mara ulisainiwa na Waziri Daniel Yona Mwaka 1999 baadaye Nazir Karamagi Mwaka 2007

32.Mh Rais mwanasheria mkuu wa serikali pamoja na makamishina wa madini Mh Andrew Chenge na Dalali kafumu walihusika ktk mikataba ya madini.

33.Makampuni ya uchimbaji yakilipwa fedha haziwekwi kwenye mabenki ya ndani badala yake huwekwa kwenye mabenki ya nje.

34.Uwekaji wa fedha kwenye mabenki ya nje badala ya mabenki ya ndani, umechochea utoroshaji mkubwa wa fedha.

35. Makapuni mengi yamekuwa hayaajiri wazawa, na mgodi mmoja ulitaka kuleta walinzi kutoka nje ya nchi.

36.Hakuna mfumo uliowekwa na serikali wa kuhakikisha kunakuwa na ufuatiliaji wa ajira zinazotolewa katika migodi nchini.

37.Sheria ya madini inatoa uhuru wa madaraka kwa Waziri wa Madini katika kuingia kwenye mikataba ya madini.

38.Mh Rais Kamati inatoa mapendekezo kuwa mikataba yote ya madini ipelekwe bungeni kujadiliwa na kisha kupitishwa kwa maslahi ya Taifa.

39.Kamati imeona hakuna haja ya kupelekwa migogoro nje ya nchi,badala yake migogoro isikilizwe hapa nchini.

40.Kamati imeona kuwa kuna uwezo wa kujenga 'smelter' hapa nchini kwa kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha kama mikopo..

 41.Licha ya kuwapo taasisi nyingi zenye dhamana ya kusimamia sekta ya madini, Tanzania imekuwa ikipata hasara kila mara.

42.Tanzania imekuwa ikipata hasara bandarini kutokana na kutokuwa na wakala wa meli.

Mapendekezo:
1.Kamati inapendekeza serikali kupitia msajili wa makampuni iichukulie hatua kampuni ya Acacia kwa kufanyakazi kinyume na sheria.

2. Serikali izuie usafirishaji wa makinikia nje ya nchi, hadi hapo wadaiwa watakapolipa madeni yao.

3.Serikali iwachukulie hatua waliokuwa Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali, Manaibu na watumishi wote waliohusika.

4. Serikali ijenge smelter hapa nchini ili kuokoa fedha zinazopotea kutokana na usafirishaji wa makinikia.

5. Serikali ichunguze mwenendo wa watumishi wa Mabaraza ya Kodi kwa kuchukua muda mrefu kutoa maamuzi ya mashauri ya kodi.

6. Sheria iongeze kiwango cha adhabu kilichoanishwa katika ukiukwaji wa sheria ya madini nchini.

7. Sheria iweke kiwango maalumu cha hisa ambacho zitamilikiwa na serikali na kuiwezesha serikali kununua hisa.

8.Sheria itamke bayana kuwa madini ni mali ya Watanzania na yamewekwe chini ya ofisi ya rais.

9. Mikataba ya madini isiwe ya siri ni lazima iridhiwe na bunge

10. Sheria iondoe mamlaka aliyonayo Waziri wa Madini na Kamishna wa Madini katika sekta ya madini.

11. Serikali ifute au kubadili sheria ya kodi ya madini ili kuondoa vifungu ambavyo havina manufaa kwa mataifa.

12. Serikali itoe elimu kwa watumishi wake kuhusu sekta ya madini.

==>Rais Magufuli anazungumza.
1.Muda mwingine ni vigumu sana huwa uzungumze nini mara baada ya ripoti hii yenye kutia uchungu sana.
2.Nisije kusahau nawapongeza kamati mmefanya kazi kubwa kwa ajili ya Watanzania wapo waliotaka kukatisha maisha yenu.

3.Nisije kusahau nawapongeza kamati mmefanya kazi kubwa kwa ajili ya Watanzania wapo waliotaka kukatisha maisha yenu.

4.Ndugu zangu watanzania Mungu alitupenda katuweka katika nchi ya Tanzania akatupatia Maliasili nyingi.

5.Nina Uhakika huko alipo shetani anatucheka nina imani shetani huyohuyo anatumia viongozi kuifanya Tanzania kuwa maskini.

6.Wakati mwingine tunapewa mikopo kwa Masharti ya ajabu ajabu huku mali tunazo sisi wenyewe jamani.

7.Kampuni inafanya biashara ya Trilioni of money lakini hata haijasajiliwa nchini mara ngapi tunawaumiza wamamchinga wasio na leseni.

8.Mali ni yangu mimi nakulinda wewe unanitisha kuwa tutashitakiwa kwa kisingizio cha ajira tuko hapa kulinda maslahi ya watanzania

9.Hawa watu muda mwingine hawana hata huruma wamechukua madini na mchanga wote huo lakini hata kodi hawakulipa.

10.Watanzania hapa Mawaziri na Wataalamu wote mioyo yao haiwaruhusu hata kwenda kukagua smelter nje ya nchi.

11.Makampuni ya kujenga smelter ya dhahabu hayaruhusiwi lakini chuma, Cement na Tiles mnaweza hili ni soko la ajabu.

12.Tulikuwa tunashare ya 15% lakini mtu akaona apunguze hii aweke asilimia 5 baadaye akaenda kuiondoa yote hiyo.

13.Yupo mpiga Kelele mmoja ambaye anapiga Kelele kila siku tulipomchunguza huko nyuma anapiga simu kwa Mwanyika anaomba data.

14.Sio kwamba mimi sina Damu ila Mungu alifawanyanyua mkaona mimi ndiyo ninafaa siwezi kuwasaliti hata kidogo.

15.Mtu kama Dkt Kafumu alikwenda kufanya forgery yupo daktari mmoja pale Muhimbili naye tulimshika hata hausiki alileta ukabila

16.Wahusika wote waliotajwa ndani ya Ripoti hii mimi nimeyakubali mapendekezo haya yote ntayasapoti kwa asilimia 100.

17.Waziri Kabudi uwe na timu ya wanasheria waaminifu, rekebisheni hizi sheria tuzipeleke bungeni zifanyiwe mabadiliko

18.Wakikiri na kuomba msamaha tutakubali kuwasajili lakini kwa sasa hakuna kuwasajili na hakuna mchanga kutoka nje

19.Wizara zote zinazohusika wawaite Acacia wawadai fedha zetu zote na wakiri walituibia. Wakikubali tutaendelea


20.Tunahitaji wawekezaji, lakini katika uwekezaji ambao utatunufaisha wote, na si wawekezaji wezi.




Muhtasari wa Ripoti ya kamati ya Rais Magufuli kama ilivyowasilishwa na Mwenyekiti wake Prof Nehemia Osoro!.

1.Kamati iliandaa mwongozo kazi,kukusanya mikataba,sheria na sera za kodi

2.Kuchambua mfumo mzima wa biashara ya makinikia!.

3,Kutembelea na kupata taarifa kutoka migodini,mamlaka ya bandari,TRA,ofisi ya takwimu,Stamico,Soko la hisa na mitaji,wizara ya nishati na madini!.

4.Kufanya mahojiano na watu kutoka serikalini na watu binafsi!.

5.Kujifunza kutoka nje ya nchi!.

6.Kufanya uchambuzi yakinifu kuhusu biashara ya makinikia tangu mwaka 1998.

7.Kufanya uchunguzi kama kuna uwezekano wa kujenga mtambo wankuchenjua makinikia!.

Matokeo

1.Acacia haijasajiliwa na inafanya biashara isiyo halali

2.Acacia haijawahi wasilisha ripoti yoyote ya kuonesha kuwa wao ni wamiliki wa migodi!.

3.Kamati imebaini Acacia wanafanya biashara kinyume na sheria ya nchi,Acacia hawajulikani kisheria.

4.Kamati imebaini Pangea na Bulyanhulu ndiyo wasafirishaji wa makinikia kutoka Tanzania na hupelekwa China,Japan na Ujerumani yakiwa kwenye makontena ya futi 20 yakiwa tayari yameshauzwa,mauzo hayo hufanya kwa mujibu wa sheria kupitia ofisi ya uhasibu iliyopo Afrika Kusini!.

5.Kamati imebaini kuwa kifungu cha 51 cha sheria ya madini kinamtaka mchimbaji apate kibali kutoka mamlaka,kamati imebaini hakuna utaratibu maalum,kifungu hiki kinataka mwekezaji kutoa taarifa sahihi!.

Kamati imebaini baadhi ya watumishi wa serikali,makampuni ya madini yametenda makosa ya jinai kwa kulisababishi taifa hasara!

Kamati pia imeridhika kuwa baadhi ya watumishi wa serikali na wawekezaji wamelitia aibu taifa kwa kutoa taarifa za uongo!.

Kamati imebaini katika kufanya biashara ya makinikia,makampuni haya yamekuwa yanafanya undanganyifu wa biashara,kutoa taarifa za uongo kuhusu idadi ya makontena na thamani yake!.

6.Makampuni ya makala ya meli yaliwasilisha taarifa za uongo kuhusu biashara ya makinikia!.

Waliruhusu biashara hii ya magendo kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu idadi ya makontena !.

7.Kamati imebaini mauzo ya makinikia hayakufanyika kwa ushindani,makinikia yaliuzwa kwa wafanyabiashara wale wale wenye mahusiano ya wawekezaji!.

Kilichouzwa hakikuwa makinikia hasa,ilikuwa ni madini hasa!.

8.Uchunguzi wa kisayansi kupitia mifumo ya kompyuta ilisababisha gharama za uendeshaji kuonekana kubwa wakati zilikuwa chini na kusabisha wawekezaji kutolipa kodi!.

9.Kamati imebaini kuwa Bulyanhulu na Pangea hawakuonesha faida wanayopata kwenye biashara!.

10.Kamati imebaini faida iliyooneshwa imekuwa ikirudishwa kwenye makampuni kama mikopo kwa kutumia riba!.

11.Kamati imebaini makinikia yaliyosafirishwa tangu mwaka 1998 kuwa makontena 44,227-61,320 sawa na shilingi Trilioni 108 za kitanzania kwa kiwango cha chini huku kiwango cha juu ikiwa ni Trilioni 180!.

Thamani ya silver toka mwaka 1998 ni shilingi bilioni 366.66,Copper ni Trilioni 2.86,surphure ni Trilioni Bilioni 277.393,Chuma ni shilingi Bilioni 368.2.,Zinc bilioni 8.42,Nicol trilion 13.22,uradium trilioni 17.19,metal Trilion 1.9.

Kifupi tangu mwaka 1998,nchi imepoteza kiasi cha Shilingi Trilion 132.56 kwa kiwango cha chini na Trilioni 200.9 kwa kiwango cha juu!.

Upande wa Makinikia serikalinimepoteza Trilion 149-253.8 
Silver ni Trilion 5,Copper trilion 3.9,Surpher,Bilioni 411,

Thamani ya madini yote kati ya mwaka 1998 hadi sasa ni shilingi Trilion 188.59-380.99

Kiwango cha mapato kilichopotea,ni Trilion 55(kodi ya mapato,Bilioni 94(Withholding tax),Mrahaba(Trilion 11) Gharama za meli Trilion (1.6)

Pesa zilizopotea zingeweza hudumia bajeti ya miaka mitatu ama kujenga reli ya standard kutoka Dsm mpaka Mwanza!

KUHUSU Makinikia

1.Kamati imebaini serikali siyo sehemu ya mkataba wa biashara ya makinikia!.

2.Mikataba haina sehemu ya masharti ya kuwataka wawekezaji kutoa taarifa za uuzwaji wa makinikia,serikali imekuwa haipati taarifa halisi

Kuhusu Mikataba ya madini

1.Kamati imebaini serikali iliingia mkataba na mwekezaji wa mgodi wa Kahama,lakini hakuna sehemu inayoonesha serikali kupata pesa za kutosha,serikali ilifikia hatua ya kupunguza hisa zake kutoka 15 mpaka 5 na kujikuta ikipata dola laki moja tu,mabadiliko haya yalifanywa na Dr Kigoda!

2.Mkataba kati ya Pangea ulisainia na Daniel Yona na Karamagi na serikami haijawahi pata chochote kutokana na kukosa hisa!.

3.Mkataba kati ya serikali ya North Mara ukiosainiwa na Daniel Yona,serikali haina hisa hata moja,mwaka 2007,serikali ilijifutia hisa zote!.

4. Mkataba kati ya GGM na serikali ulisainiwana Daniel Yona,hapa napo serikali haina hisa hata moja!.

5.Kamati imebaini kuwa kumekuwa na uongezwaji wa mikataba inayofanywa na serikali,waliohusika ni Willium Ngereja,Prof Muhongo,wanasheria wa serikali!.

6.Kamati imebaini kuwa sheria haizuii serikali kubadili sheria na sera!

7.Kamati imebaini mikataba inaweza kurekebishwa kwa maslahi ya taifa/nchi!.

8.Kuhusu misamaha ya kodi,kamati imebaini misamaha inayosababisha hasara!.

9.Kamati imebaini kuwa makampuni haya yamekuwa hayaweki fedha kwenye mabenki ndani!.

10.Kamati imebaini makampuni haya kuajiri wazawa kwenye maeneo yenye wataalam,kamati imebaini kuwa hakuna utaratibu madhubuti uliowekwa na serikali kuhakikisha kigezo hiki kinatekelezwa!.

11.Kamati imebaini kuwa makampuni yamekuwa yakichangia kiasi kidogo kwenye shughuli za maendeleo ya jamii!.

12.Kamati imeona kuwa waziri amekuwa na madaraka makubwa,kamati imebaini kuwa bunge lipewe nguvu na siyo waziri pekee!.

13.Kamati imependeleza sheria ya madini ifanyiwe mapitio!.

14.Kamati imebaini kuwa nchini inaweza kujenga mtambo wa kuchenjua makinikia hapa nchini!.

14.Kamati imebaini kuwa nchi haina taasisi zinazosimamia biashara ya madini,tangu serikali iivunje Nasaco makampuni ya usafirishaji yamekuwa yakifanya kazinya Nasaco(yanajikagua yenyewe).

MAPENDEKEZO YA KAMATI

1.Hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya Acacia

2.Serikali idai kodi na makampuni yote yaliyokwepa kodi!.

3.Usafirishaji wa makinikia usitishwe mpaka kodi ilipwe

4,Mtambo wa kuchenjua makinikia ujengwe!.

5.Waliohusika wote katika kuingia mikataba wachukuliwe hatua za kisheria!.

6.Utaratibu wa malipo ya mrahaba ufutwe!.

7.Serikali ifanye uchunguzi kuhusu mwenendo wa watumishi wa mabaraza ya kodi!.

8.BOT ifuatilie malipo ya mrahaba

9.Serikali ianzishe utaratibu wa ulinzi kwenye migodi

10.Adhabu za waliokiuka sheria ziongezwe!.

11.Mikataba yote ya madini ipitiwe upya!.

12.Sheria iweke kiwango maaluma cha hisa!.

13.Serikali iunde chombo cha kusimamia ustawishaji wa biashara!.

14.Sheria iseme madini ni malinya watanzania chini ya udhamini wa rais

15. Mikataba yote iwe wazi

16.Madaraka ya waziri na kamishna yapunguzwe!.

17.Suala la ajira na mafunzo kwa wazawa izingatiwe!.

18.Fedha za mauzo ya madini ziwekwe kwenye mabenki!.

19.Serikali ifute ama izifanyie marekebisho kwenye sheria za kodi na madini!.

20.Serikali itoe mafunzo ya mara kwa mara kwa watumishi wake!.

21.Serikali iwe inafanya ukaguzi wa mara kwa mara!
 SIKILIZA HAPA 


No comments: