Sunday, June 25, 2017

TID AMTAKA QUICKROCKA AMLIPE MIL.20 KABLA HAJAMFANYIA KITU KIBAYA

Leo June 24, 2017 upepo wa Bongofleva huenda ukaenda sivyo kwenye studio za Switch Records ikiwa ni masaa tu tangu Quick Rocka na kundi la OMG waachie video yao mpya “Watasema” ambayo wametumia melody na maneno ya wimbo wa zamani uliofanywa na TID “Watasema Sana” na inaonekana TID hajashirikishwa na kuamua kudai haki zake.

TID ameandika >>> “Wat is this….?! Hivi ndio mnapata Magari yenu!? @quickrocka & @omgtanzania we need to TALK #Watasema
Naomba tukutane Central Police huwezi kutumia Haki zangu hivihivi Kabla sijafanya kitu kibaya nahitaji million 20 compensation… This song ni Awards mbili Za Kisima Music Awards 2005 in Kenya u can’t just Steal it, Unalala Ndani Leo<<< – TID

No comments: