Wednesday, June 14, 2017

Wafanyakazi wa Kampuni ya Bima ya Resolution wachangia Damu

Wafanyakazi wa kampuni ya bima ya Resolution wachangia damu. Hii ni katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya uchangiaji damu. Akizungumza wakati wa zoezi hilo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya bima ya Resolution Bi. Mary Anne Mugo alisema kuwa mchango huo upo ndani ya viupaumbele vya kampuni hiyo, kusaidia jamii katika maeneo mbalimbali ikiwemo afya za watanzania.
“Tupo katika utaratibu wa kawaida wa kuwajibika kwa jamii na dhumuni ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuhakikisha benki ya damu nchini inakuwa na akiba ya kutosha” alisema Mugo.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya bima ya Resolution BI. Mary Anne Mugo akishiriki zoezi la uchangiaji damukama mchango wake kwenye maadhimiso ya siku ya uchangiaji damu duniani. Zoezi hilo limefanyika makao makuu ya kampuni hyo jijini Dar es Salaam.

Wafanyakazi wa kampuni ya bima ya Resolution wakishiriki zoezi la uchangiaji damu kama mchango wao kwenye maadhimiso ya siku ya uchangiaji damu duniani

Mfanyakazi wa kampuni ya bima ya Resolution, Bi. Rose Ngowi akishiriki zoezi la uchangiaji damu.


Mfanyakazi wa Kampuni ya Bima ya Resolution, Bw. Marcelino Mitawa akishiriki zoezi la uchangiaji damu

Mfanyakazi wa Kampuni ya Bima ya Resolution, Bi. Namshalu Kisimbo akishiriki zoezi la uchangiaji damu

Mfanyakazi wa Kampuni ya Bima Resolution, Bw. Godfrey Adialo akishiriki zoezi la uchangiaji damu

No comments: