Saturday, August 5, 2017

ANGALIA HAPA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI WAKIPEWA SEMINA KWENYE MAANDALIZI YA TAMASHA LA JINSIA

Leo ikiwa ni tarehe 5 mwezi 8 Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) umewakutanisha wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mwanaharakati mkongwe Mama Gertrude Mungella, lengo likiwa ni kujadili harakati za ukombozi wa wanawake kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Bi. Lilian Liundi akiongea na Wahariri wa vyombo vya habari mapema leo, kwenye Semina ilifanyika kwenye ukumbi wa mtandao huo Mabibo jijini Dar es salaam
Akiongea kwenye semina hiyo mkurugenzi mtendaji wa TGNP mtandao Bi. Lilian Liundi alisema kubwa zaidi ni Tamasha la Jinsia linalotarajiwa kufanyika tarehe 5 mpaka 8 ya mwezi wa 9 kwenye viwanja vya mtandao huo. Na Tamasha hilo litawakutanisha zaidi wanawake 1000 toka maeneo mbalimbali lengo likiwa ni kusherekea mafanikio pamoja na kuzijadili changamoto zinazowakabiri wanawake na namna ya kuzitatua.
Lakini pia kujadili mambo mbalimbali yanayowakabiri  wanawake Kiuchumi kama kuzitafuta fursa na namna ya kuzitumia endapo watazipata. Pamoja na sera ya serikali ya viwanda kufahamu wanawake wamejipanga vipi kwa hili na lengo likiwa ni wanawake kumiliki viwanda vyao na siyo kufanya kazi za kuzalisha kwenye viwanda vya wengine.
Baadhi ya wahariri wakisiliza kwa makini wawezeshaji wa Semina iliyoandaliwa na mtandao wa jinsia TGNP Mapema leo jijini Dar es salaam
Na pia kutakuwa na wanawake mbalimbali ambao wamefanikiwa kuwawakilisha wenzao kwenye Nyanja mbalimbali kama Mama Gertrude Mungella, Spika mstaafu Anna Makinda, Makamu wa Rais Samia Suluhu n.k wakijaribu kutoa shuhuda zao walipoanza harakati mpaka kufikia mafanikio ili kuweza kuwashawishi na wanawake wengine kuthubutu kufanya kama wao. Lakini pia bila kusahau mchango wa wanawake waliofanya vizuri na kwa sasa wameshafariki kama Bibi Kidude binti Baraka, Bibi Titi Mohamedi na wengine wengi.
Pia kuangali mikataba mbalimbali ya kikanda na  yakimatifa ambayo serikali yetu imeingia ambayo inaonyesha kupinga ukatili dhidi ya wanawake na jinsi ya kuwezesha wanawake na kiuchumi, kisiasa na kijamii kama utekelezaji wake unafanyika ipasavyo.
Mama Gertrude Mungella akiongea na wahariri kwenye Semina iliyoandaliwa na TGNP Mtandao mapema leo jijini Dar es salaam
Wajasiriamali toka mikoani nao watapata nafasi ya kuja kutambulisha bidhaa zao na kujifunza jinsi ya kupaki bidhaa zao za vyakula na nyinginezo, ili kuweza kupata soko kubwa la ndani na hatimae kuingia kwenye ushindani wa soko la kimataifa kimataifa.
Wadau mbalimbali toka serikalini watakuwepo kuja kuchukua mapendekezo ya wajasiriamali pamoja na kutoa ushauri nini wafanye ili waweze kufanikiwa. Lakini  pia kuzungumza na wanawake kuhusu changamoto zinazowakabiri na namna ya kufanya utatuzi wa changamoto hizo.
Mama Gertrude Mungella akionge mbele ya kamera za waandishi wa habari kwenye semina iliyoandaliwa na Mtandao wa Jinsia (TGNP) leo jijini Dar es slaam
Kwa upande wake Mama Gertrude  Mungella alipenda kuwashauri wahariri na waandishi waliofika kwenye semina hiyo. kuweza kuwapa nguvu wanawake kupitia vyombo vyao vya habari na siyo kuwafedhehesha hali inayowafanya wanawake wengi kujiona wao ni watu wa chini. Hali inayowafanya wanawake wengi kujiona hawawezi kufanya mambo makubwa katika jamii yao.
Lakini pia alipenda kuwashauri TGNP na wadau wengine wote juu ya matumizi mazuri ya vyombo vya habari “media ukizitumia vizuri zinaweza kukufikisha pazuri lakini ukishindwa kuzitumia pia zitaharibu malengo na kile ulichokikusudia na baadae utalaumu wamekuandika vibaya hali ambayo siyo nzuri”.alisema Mama Mungella 
Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa mtandao wa jinsia 
Na mwisho alipongeza jitihada zinazofanywa na Mtandao wa Jinsia Tanzania kuwa kuendeleza harakati za ukombozi wa mwanamke, kwani bila wao mambo mengi yangesahaulika na hata wao waliojenga historia wasingeendelea kujulikana kama sio kuitwa kwenye shughuli kama hizi.




No comments: