Tuesday, September 12, 2017

KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU KIMEENDESHA WARSHA YA KUPINGA UKEKETAJI NCHINI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetakiwa kuweka sharia madhubuti za kuwaadhibu watu wanaondeleza vitendo vya ukeketaji kwa  wanawake kote nchini.
Hayo yamesemwa mapema leo katika warsha iliyoandaliwa na Kituo cha Sharia na Haki za Binadamu yenye lengo la kupinga ukeketaji na kutokomeza kabisa vitendo vya ukeketaji kwa wanawake na wasichana.

Akiongea na waandishi wa habari kiongozi mkuu wa timu ya watafiti Dr. Geofrey Chambua alisema kuwa wao utafi wao umelenga zaidi kwa wanawake wenye umri wa miaka 18 na kuendelea kwani kundi hilo ni kama limewekwa pembezoni.

Alisema kuwa utafiti huo umefanywa katika mikoa mitatu ambayo ni vinara kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Tume ya Taifa ya Utafiti ambayo imeonyesha kuwa mkoa wa Manyara unaongoza kwa kuwa na  58%  Mara 32% na Singida 31.
Aliendelea kusema kusema kuwa kundi la umri wa miaka 15 – 19 ni asilimia 5 peke yake na kundi lililobaki la kuanzia miaka 20 na kuendelea ni lenye tatizo kubwa zaidi, na wao wanahisi ni kutokana na kuwa sharia inawalinda watoto hao na hao wengine hakuna sharia inayowalinda.

Lakini jambo lingine ni wananchi kuwa waoga wa kutoa taarifa endapo wanatendewa vitendi hivi lakini pia wazazi au walezi wanaogopa kutengwa na familia au jamii kwa kutoa ripoti polisi kwa kuwa ni utamaduni wao.

Na lingine kwa hawa wenye umri wa miaka 20 na kuendelea ni watu wazima wanaojitambua lakini pia ukubali kukeketwa kwa sababu ya kupata fursa sawa na wengine kwani mwanamke asiye keketwa utengwa na jamii nzima na pia kukosa mume kwa kuonekana kuwa hajakamilika.
Aidha dr. chambua alipenda kushauri vyombo husika vya maamuzi kama bunge kutunga sharia zinazolinda makundi yote na siyo kuangali kundi la mabinti wenye umri mdogo peke yake kwani kitendo cha kumfanyia ukeketaji mwanamke ni kumkosesha haki yake kimsingi.

Lakini pia kwa mashirika yasiyo ya kiserikali na yanayohusika na haki za mwanamke na mtoto pamoja na jamii kwa ujumla kuungana kwa pamoja kusambaza elimu hii kuondoa tatizo la ukeketaji.
Bila kusahau kundi muhimu la Viongozi wa dini zote na madhehebu yote kuweza kushirikiana kwa pamoja kutoa elimu hii kwa waumini ili waache kukeketa kwa kujua siyo jambo zuri la kufanyiwa mwanamke wa umri wa wowote.




No comments: