Thursday, October 19, 2017

ANGALIA HAPA WAFANYA BIASHARA WA MIPAKANI WAPATA MAMBO MAZURI KAMA HAYA SIKU YA PILI YA SEMINA

Wafanya biashara wa mipakani wametakiwa kuwa wabunifu na wenye hekima na kauli nzuri zitakazo wavutia wateja wao, na kujaribu kuchunguza soko linahitaji nini kwa wakati iliopo kabla ya kupeleka bidhaa sokoni.  
Hayo yamesemwa na mwalimu wa biashara na masoko kutoka chuo cha biashara CBE Bi. Rehema Tambwe alipokuwa akiongoza warsha ya mafunzo kwa wafanya biashara wa mipakani mapema leo jijini Dar es salaam.

Warsha hiyo itakayodumu kwa muda wa siku tatu imelenga kuwajenga wafanya biashara wanawake wa mipakani kwa kuwapa elimu itakayowaongoza kufanya biashara zao kwa uhuru, uwazi na kwa kujiamini kwa kuwa wanazijua sharia na haki zao za msingi wafikapo katika mipaka hiyo.
Bi Rehema alisema kuwa wafanya biashara wengi wamekuwa waoga kuhoji wafikapo mipakani hivyo kusababisha kupoteza haki zao za msingi, na hii sio kwa wale ambao hawajapata elimu bali hata kwa wale waliosomea mambo haya ya biashara wakifika eneo hilo utetemeka na hivyo wasimamizi wa hapo wanawapeleka wanavyotaka wao.

Na hii inatokana na kutoamini bidhaa yako ama kile ambacho unakwenda kukifanya katika hiyo nchi unayokwenda kwani ukiwa na bidhaa nzuri imewekwa katika vifungashio vizuri na pia unajua sharia za umoja wa soko la Afrika Mashariki hautapata tabu ya kuyumbishwa na yeyote na wala haitakulazimu kuhitaji kutumia njia za panya.
Lakini pia wafanya biashara wengi wanafanya biashara bila kufanya uchunguzi wa kuangalia soko linahitaji nini kwa sasa, ama huku ninapopeleka bidhaa wateja wangu ni wakina nani na matokeo yake wanajikuta wanapeleka bidhaa ambazo zipo kwa wingi katika eneo hilo na inawezekana zikawa na ubora mkubwa kuliko za kwao na kusababisha kutonunuliwa kwa bidhaa hazo.

Muwezeshaji aliendelea kusisitiza swala la ubunifu ni muhimu katika biashara kwani mnapokuwa wafanya biashara wengi kinachoweza kukutofautisha wewe na wengine ni ubunifu wako katika bidhaa hata katika muundo wako wa kutoa huduma unahakikisha kuwa unafanya kitu cha ziada kuhakikisha wateja wanaacha kwenda kwa wengine na wanakuja kwako.
Na jambo lingine alilolisema muwezeshaji ni kuongeza Thamani katika bidhaa na hii inatokana na jinsi ya kuziweka bidhaa zako kwa mfano wauzaji wa batiki unapozitengeneza batiki zako unatafuta vifungashio vizuri unaziwaka hata mteja akija anazidi kuziona mpya na siyo unaweka kwenye msumari tu zinakuwa na vumbi mpaka mteja akitokea zinakuwa zimesha chakaa inamlazimu aende akafue ndipo aweze kuivaa.

Bi Rehema aliendelea kusisitiza kuwa biashara inatakiwa kujiendesha yenyewe na sio majukumu yako binafsi ukayaingiza katika pesa ya biashara kwani utaanguka tu, kwa waliowengi wanachukulia fedha zote ni za kwao kwaiyo wanafanya matumizi bila kujua kuwa wanadidimiza mtaji kwa kuitumia pesa ya biashara katika matumizi binafsi na matokeo yake umepeleka bidhaa nchi jirani lakini unarudi msingi ukiwa umepungua.

Na mwisho kabisa ni swala la mapokezi kwa mteja na kutumia lugha nzuri kwa mteja itakayomshawishi kununua bidhaa hata kama ajapanga kununua bidhaa hiyo, kwani ukimpokea vizuri na kwa unyenyekevu na kumpa maneno matamu atavutiwa na biashara yako na atakuletea wateja wengi zaidi na hii ni kwa kuona ukarimu wako katika biashara.

No comments: