Thursday, October 19, 2017

CDF WAJA NA “TUWEZESHE “KATIKA KUWAPA WASICHANA UWEZO WA KUWA VIONGOZI.


Taasisi ya Children Dignity Forum (CDF) wazindua mradi wa “Tuwezeshe” unaolenga kuwapa uwezo wasichana kuwa viongozi na wajasili katika kutatua changamoto zinazowakabili katika mustakabali wa maendeleo yao.
Mkurugenzi Mtendaji wa CDF Bw.Koshuma Mtengeti akizungumza na wanufaika wa mradi huo mara baada ya kumaliza mafunzo hayo
Akitoa taarifa hiyo jana jijini Dar es salaam katika ukumbi wa Double View,Mkurugenzi mtendaji wa taasisi hiyo Bw.Koshuma Mtengeti amesema ili kumpa uwezo wa kuongoza mwanamke basi ni lazima awe jasili na mwenye kuweza kukabiliana na changamoto na hilo ndio lengo kuu la mradi huo.

“lengo kubwa la project hii ni kumpa uwezo msichana kuwa kiongozi jasili na mwenye uwezo wa kukabiiana na changamoto”.alisema.

Aidha,Bw.Mtengeti amesema mradi huo ulioanzishwa mwaka huu utadumu kwa miaka 4 ukiwa na wasichana 16 toka mikoa ya Dar es salaam na Mwanza utawasaidia wasichana kuwa viongozi majasili na wenye kuweza kutatua changamoto ambazo mara nyingine zimekuwa zikikatisha ndoto zao.
Mwenyekiti wa bodi ya CDF Bi. Fortunata  Temu akitoa neno kwa washiriki 16 ambao watahusika na mradi wa Tuwezeshe.
Pia, Mwenyekiti wa Bodi ya CDF, Bi.Fortunata Temu aliwataka wasichana wote waloshiriki katika mafunzo ya mradi huo wakatekeleze yale walojifunza kwani huo ndio msingi katika kufikia maadhimio ya mradi.

“Nawaombeni sana wote mloshiriki mafunzo haya yasiishie hapa mkafanye yale mlofundishwa kwani huo ndio msingi mkubwa wa maadhimio ya mradi huu.”alisema.

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo ya mradi huo akiwemo Bi.Lulu Urio,Mariana Mubelwa na Euphoria Edward wamewashukuru wale wote walioandaa mafunzo hayo wakiwemo FORWARD UK, AMWA na Mwenyeji CDF kwa kuweza kuwaletea mradi huo kwani wanaamini ni kama wamezaliwa upya baada ya kupata mafunzo hayo kwani mbali ya kuongeza marafiki wapya ila kuna kitu kipya kimeingia ndani ya vichwa vyao na wanaamini havitafutika kamwe mana sasa wamekuwa majasili na kuweza kusimama na kuongea mbele za watu bila hofu tofauti na awali.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wao wa CDF, Forward Uk na Amwa baada ya kumaliza mafunzo hayo.

Hata hivyo,Mradi huu wa “Tuwezeshe” umeanzishwa mwaka jana 2016 katika nchi za Uingeleza,Uganda,Kenya,Somalia na mwaka huu ni Tanzania kupitia Taasisi isiyo ya kiserikali inayosimamia haki za watoto na kuwawezesha wasichana (Children Dignity Forum).

No comments: