Saturday, October 7, 2017

Kijana Huyu ameahidi kumuua Lissu akirejea matibabuni-soma Hii

Kijana alyeahidi kummaliza Lissu akirudi kutoka kwenye matibabu

Mkurugenzi wa Oganaizesheni, Mafunzo na Uratibu wa Kanda, Benson Kigaila amefunguka na kulilalamikia jeshi la polisi kushindwa kumkamata ki...
 Yatakayo jadiliwa kikao cha CCM kesho Zanzibar
 Kamanda wa Polisi Geita amekuja na taarifa hii kukamatwa kwa mbunge Msukuma
 Taarifa ya Kamanda Mambosasa waliokamatwa mkutano wa kumuombea Lissu
Mkurugenzi wa Oganaizesheni, Mafunzo na Uratibu wa Kanda, Benson Kigaila amefunguka na kulilalamikia jeshi la polisi kushindwa kumkamata kijana ambaye anaendelea kuandika vitisho kwenye mtandao wa jamii juu ya Tundu Lissu. 
 
Kigaila amesema kuwa kabla ya Mbunge wa Singida Mashariki kupigwa risasi Septemba 7, 2017 mjini Dodoma huyo kijana kupitia mitandao ya kijamii aliomba apewe ruhusa ya kumuuwa Lissu kwa mikono yake mwenyewe. Kigaila amedai kuwa kijana huyo hivi sasa ameendelea kuandika ujumbe mbaya zaidi kupitia mitandao hiyo hiyo ya jamii bila ya polisi kumchukulia hatua zozote zile. 

"Sasa huyo kijana anaandika vibaya zaidi anasema 'Anasikitika sana kwa mtu aliyefanya hilo tukio la kumpiga Lissu anasema alitegemea asikie Lissu amekufa siyo kwamba Lissu amejeruhiwa na anasema wanamsubiri Lissu atakaporudi Tanzania mara hii hawatafanya kosa, wanasema walifanya kosa Dodoma sasa huyu mtu awe ni yeye kweli au si yeye aliyefanya tukio hilo, awe ni mwendawazimu au si mwendawazimu tulitegemea polisi wawe wameshamkamata wapo naye wanamuuliza haya anayosema ni kwa sababu gani lakini polisi halimuoni huyo kijana" alisema Kigaila 

Aidha Kigaila amesema kuwa kitendo cha polisi kutomchukulia hatua kijana huyo kinazidi kuwapa mashaka kuwa huenda wanamtambua huyo kijana lakini hawataki kumkamata kwa sababu zao binafsi.

No comments: