Saturday, October 14, 2017

NAIBU WAZIRI WA AFYA NDUGULILE AZINDUA KITUO CHA AFYA PEMBA MNAZI KIGAMBONI DAR ES SALAAM

Hospitali na zahanati za manispaa ya kigamboni zimeendelea kufanya vizuri katika utoaji wa huduma za afya hadi kufikia kuwa na kiwango cha nyota tatu japo kuwa halmashauri yake bado ni changa.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

 Dr. Faustine Ndugulile akizindua kituo cha afya cha Pemba Mnazi wilaya ya Kigamboni jijini Dar es salaam.

Hayo yamesemwa mapema leo na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto Mh. Faustine Ndugulile alipokuwa akizindua kituo cha afya cha Pemba Mnazi kilichopo halmashauri ya manispaa ya Kigamboni jijini Dar es salaam.

Katika  uzinduzi huo wakazi wa eneo hilo walipata nafasi ya kutoa kero zao mbele ya naibu waziri na miongoni mwa malalamiko hayo ni upungufu wa Zahanati, vifaa tiba kama mashine za X-ray pamoja na Outro sound, magari ya wagonjwa, mashimo ya kutupia taka taka n.k
Mkuu wa wilaya ya kigamboni Mh Hashim Mgandilwa akimkaribisha naibu waziri wa afya, 

Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

 katika uzinduzi wa kituo cha afya cha Pemba Mnazi manispaa ya Kigamboni jijini Dar es salaam.

Lakini pia changamoto nyingine ni ubovu wa bara bara hali inayofanya kushindwa kupitika wakati wa mvua pamoja na upungufu wa watumishi katika kituo hicho alichokizindua leo kwani kina jumla wa watumishi wawili ambao ni mganga mmoja na muuguzi mmoja.

Akijibu maswali ya wakazi hao naibu waziri huyo alisema kuwa kwa sasa tatizo la madawa halipo kwa zaidi ya asilimia 80 kwani serikali imetenga fedha za kutosha kuhakikisha dawa zinapatikana katika hospitali za serikali na wagonjwa hawalalamiki tena kuhusu madawa kwani bohari ya taifa ya madawa ina dawa za kutosha.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

 Dr. Faustine Ndugulile akiongea na wakazi wa pemba mnazi katika uzinduzi wa kituo cha afya kilichopo kata ya Pemba Mnazi Kigamboni jijini Dar es salaam.
Lakini pia Dr. Faustine alisema kuhusu tatizo la umeme ametoa maagizo kwa mkurugenzi wa manispaa kuwasiliana na mkurugenzi wa Taneso ili jumatatu waje wafanye tathini ya kiwango gani kinahitajika ili atoe na huduma hiyo iendelee kupatikana kituoni hapo.

Aidha naibu waziri huyo aliendelea kusema kuwa hospitali ya Vijibweni pale ilipo ni padogo hivyo kuna eneo lililotengwa kwa ajiri ya ujenzi wa hospitali hiyo na mwakani mwanzoni ujenzi huo utaanza na kwa vifaa tiba kama X ray ataongea na wizara yake mpaka mwakani mashine hizo zitakuwepo ili kuepuka tatizo la kwenda mpaka wilaya nyingine kufuata huduma hizo.

 

No comments: