Thursday, October 5, 2017

SIMBANET KUTANGAZA FURSA KWA VIJANA WATANZANIA

TANZANIA ikiwa  kwenye mapinduzi ya kiteknolojia ilhali  inadaiwa kuwepo kwa changamoto ya ajira ambapo mapunduzi hayo yanaweza kutoa fursa zaidi.

Fursa hizo zimeelezwa kuwa zipo kwenye teknoljia endapo vijana hao watajitambua kwa kufanya kazi vizuri katika kuitumia mitandao ya kijamii kwa ufanisi.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa  Operesheni  kwenye mtandao wa Simba Net wa Tanzania Kenya na Uganda, Hussein Kitambi, amesema kuwa Simba Net itawakutanisha vijana  100 watakao funguliwa fikra ya jinsi Teknolojia inavyoweza kuwasaidia kujipatia ajira,
 
Amesema kuwa mkutano huo utakaofanyika kesho jijini Dar es Salaam katika  Ofisi za  Umoja wa Mataifa ambapo Simba Net ikishirikiana na wadau mbalimbali wa Teknolojia.

No comments: