Wednesday, November 15, 2017

MUME WA ZAMANI WA UWOYA NDIKUMANA AFARIKI DUNIA JUA SABABU ZA KIFO CHAKE HAPA...

                                 Tokeo la picha la ndikumana
Aliyekuwa  mume wa muigizaji wa filamu nchini, Irene Uwoya, mchezaji Hamad Ndikumana (39) kutoka nchini Rwanda amefariki usiku wa kuamkia leo, chanzo cha kifo chake kikisemekana ni matatizo ya moyo ambapo jana alikuwa akiendelea na kazi zake kama kawaida.

Mpaka anakutwa na umauti alikuwa akicheza katika timu ya APOP Kinyras Peyias FC ya  Cyprus.  Alizaliwa Oktoba 5, 1978 na mpaka anafariki dunia alikuwa ametengana na Uwoya kwa mingi na alikuwa ndiye mkewe waliyefunga naye ndoa katika Kanisa Katoliki na walibahatika kupata mtoto mmoja  ambaye jina lake ni Krish.

No comments: