Saturday, December 30, 2017

JULIANA SHOZA ATOA ONYO HILI KWA WASANII WA BONGO

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Juliana Shonza amesema wizara yake haitasita kumchukulia hatua msanii yeyote ataekaidi agizo la kuvaa mavazi yenye staha.
 Picha inayohusiana
Naibu Waziri huyo ameyasema hayo katika uzinduzi wa Tamasha la Tanzania Tukuza Utalii Festival lenye lengo la kukuza utalii lililoandaliwa na Shirikisho la Waimbaji wa Nyimbo za Injili chini.

“Wasanii wote ambao wataendelea kukaidi agizo la mheshimiwa Rais la kutokuvaa mavazi ya staha Wizara yangu haitawavumilia tutachukua hatua kwa yeyote bila kujali nafasi au umaarufu wake, kabla dhoruba haijawakumba wabadilike, kwenye kupiga rungu siangalii mtu usoni.,”amesema Naibu Waziri Shonza.

Siku chache zilizopita Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli wakati akihutubia Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi CCM alitoa tamko la kuwataka wasanii kuvaa mavazi ya heshima katika video za nyimbo zao.

No comments: