Friday, December 29, 2017

Wateja wa Tigo Pekee Wanafurahia Bonasi za Bure kwa Bando Zote

                                        Tokeo la picha la tigo logo
Tofauti na taarifa zilizochapishwa zinadozai kuwa Tigo ndio mtandao wenye gharama kubwa zaidi, Tigo ingependa kuwataarifu kuwa wateja wetu wanafurahia mojawapo ya gharama nafuu zaidi nchini.

Bando zetu zinaanzia TZS 500; hakika wateja wa Tigo wanaonunua bando ya sauti ya TZS 500 kupitia menu yetu mpya ya 147*00 wanapata dakika 16. Pamoja na hili, wateja wa Tigo wanaonunua bando hii wanapokea bonasi ya dakika tano (5) BURE kila mara wanaponunua bando hii kupitia promosheni ya TUMEKUSOMA ambayo inawapa jumla ya dakika 21. Kwa hiyo kwa bando la TZS 500, bei zinaweza kufikia TZS 17.2 kwa dakika bila kujumuisha kodi.

Bando ya TZS 1000 inayonunuliwa kupitia *147*00# inawapa wateja wetu dakika 55, ambapo pia wanapokea bonasi ya dakika 30 BURE kupitia promosheni ya TUMEKUSOMA. Hii inawapa jumla ya dakika 85; kwa hiyo bei inaweza kufikia TZS 8.5 kwa dakika bila kujumuisha kodi.

Tigo inajulikana kwa promosheni kabambe na ubunifu wa ofa. Tigo pia imejijengea jina kama mtandao unaowaelewa zaidi wateja wake na kuwapa bidhaa zinazoendana na mahitaji ya soko.

Wateja wa Tigo ndio watumiaji wa simu pekee wanaopokea bonasi za bure kwa kila bando wanayonunua, hivyo kuhakikisha kuwa wateja wa Tigo wanafurahia huduma bora zaidi kwa viwango bora na nafuu nchini.

Kupitia huduma zake za kipekee za sauti, ujumbe mfupi, intaneti yenye kasi ya juu ya 4G na huduma za kifedha kupitia simu za mikononi, Tigo inaongoza kwa ubunifu wa kidigitali ikiwemo;
  • Tigo Halichachi ndio bando ya kwanza iliyowezesha wateja wa simu nchini kutumia bando zao za simu bila muda wa ukomo wa matumizi.
  • Kuwa kampuni ya kwanza ya simu kuzindua simu za Smartphone zenye lugha ya Kiswahili
  • Kuwa kampuni ya kwanza ya simu kuzindua Facebook ya bure kwa lugha ya Kiswahili
  • Kampuni ya kwanza ya simu kuzindua huduma za fedha kupita smart apps
  • Huduma ya kwanza yenye uwezo wa kubadili thamani ya fedha kwa sarafu ya nchi husika Afrika Mashariki iliyowezesha wateja kufanya miamala ya uhakika ya fedha kupitia simu za mkononi kwenda nje ya nchi.     

Tigo pia inajivunia mtandao mpana, wa uhakika zaidi wa 4G nchini, uliosambaa katika miji 24 Tanzania, hivyo kuwawezesha wateja kufurahia maisha ya kidigitali.

No comments: