Tuesday, March 27, 2018

SHIKA NDINGA MWAKA 2018 YAENDA SAMBAMBA NA MIAKA MINNE YA EFM RADIO

Kituo cha radio cha Efm chenye makao makuu yake Kawe jijini Dar es salaam mapema leo kimekutana na waandishi wa habari lengo likiwa ni
kujadili mambo makubwa mawili.
Magari ya washindi wa mwaka jana wa shindano la shika ndinga mwaka 2017.

Akiongea katika mkutano huu Meneja Mkuu wa Efm radio na Tv E Bw. Dennis Busulwa alisema kuwa lengo kuu la mkutano huo ni kuufahamisha uma kuwa mpaka kufikia tarehe 2 ya mwezi 4 mwaka huu kituo hicho kinatimiza miaka minne tangu kuanzishwa kwake.

Aliongeza kuwa mbali na sherehe hizo za kutimiza miaka minne lakini pia wako katika mpango kabambe wa kulitangaza shindano lao la shika ndinga mwaka 2018 lotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Aidha meneja Busulwa alisema kuwa katika sherehe hizo za miaka minne ya kituo hicho wataweza kuongeza masafa yao katika mikoa mingine minne ambayo ni Dodoma, Morogoro, Tabora na Kigoma.

Meneja huyo wa Efm alisisitiza kuwa mpaka sasa kituo chao cha matangazo kimekuwa cha kwanza kusikilizwa ndani ya mkoa wa Dar es salaam kwa utafiti uliyofanywa na mashirika binafsi na ni cha pili kusikilizwa kwa maeneo ambayo matangazo yao yanafika.

Ikimbukwe kuwa mpaka sasa Efm inasikika katika mikoa sita ambayo ni Dar es salaam, Pwani, Mbeya, Mtwara,Tanga na Mwanza  na mpaka kufikia siku hiyo ikiwashwa na hiyo minne itakuwa inasikika katika mikoa kumi ndani ya Tanzania.

Kwa upande wa shika ndinga 2018 safari hii mikoa itaongezeka siyo kama ilivyozoeleka kuwa washiriki wanatoka Dar es salaam na Pwani peke yake.

“Kwa mwaka huu wa 2018 shika ndinga itafanyika katika mikoa sita ambayo ni Dar es salaam, Mtwara, Mbeya, Tanga, mwanza na Pwani na kila mkoa zitaweza kutolewa pikipiki mbili na washiriki wa mikoani watagharamiwa na nauli kuja kushiriki fainali itakayofanyika jijini Dar es salaam” alisema Meneje Busulwa

”Katika haya mashindano ya mwaka huu yataweza kuwa na ubunifu tutaweza kumpata mshindi mmoja wa kiume na mmoja wa kike ambao watapewa zawadi ya virikuu kila mmoja, lakini pia washindi wa pili watapewa boda boda kila mmoja hii ikiwa ni njia yetu ya kuwawezesha wasikilizaji wetu katika Nyanja ya uchumi” aliongezea Meneja Busulwa

Na wadhamini wakubwa wa shika ndinga mwaka 2018 ni Shirika la simu  la TTCL, Tatu Mzuka na Chotec wasambazaji wa vilainishi vya shell Advance lakini pia watu watakao shiriki pamoja katika kuadhimisha miaka minne ya Efm radio pamoja na TVE.


Meneja Mkuu wa Efm Radio pamoja na Tv E Bw. Dennis Busolwa akitoa maelezo mafupi kuhusu shidano la Shika Ndinga 2018 pamoja na miaka minne ya Efm Radio.
Meneja Uhusiano wa shirika la simu la TTCL Bw. Nicodemus Tom akitoa ufafanuzi kuhusu bidhaa zao.
Baadhi ya wafanyakazi wa Efm Radio pamoja na Tv E wakifuatilia mkutano 
Mkurugenzi Mtendaji wa Chotec Bw.Choba John Mumba akitoa ufafanuzi juu ya mahusiano yao na kituo cha utangazaji cha Efm radio.
Afisa Mahusiano wa Tatu Mzuka Bi. Patronila Mtatiro akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mapema leo jijini Dar es salaam.
Mkutano ukiendelea.
Mshindi wa Shindano la Shika Ndinga mwaka 2017 Bw. Michael Peter akitoa ushuhuda kwa namna alivyoweza kushinda shindano hilo.
Mshindi wa kike wa shindano la Shika Ndinga Mwaka 2017 Bi. joyce Daniel akitoa ushuhuda kwa namna alivyoshinda na amepata faida gani toka ashinde shindano hilo.

No comments: