Thursday, March 29, 2018

TECNO KUZINDUA TOLEO JIPYA?

Paparazi tayari wameshaanzisha uvumi kama ilivyo ada, ambapo safari hii wakiihusisha kampuni kinara katika uzalishaji wa simu za mkononi TECNO,ikitajwa zaidi midomoni mwa watu, tetesi zaidi zinaihusisha kampuni hiyo pendwa na ujio wa toleo jipya ikiwa ni muendelezo wa jamii ya Camon inayosemekana kuzinduliwa nchini Nigeria, siku na saa bado havikuwekwa wazi.
Inasemekana kwamba simu hiyo itaendana na uchumi wa Afrika ikikadiriwa kuwa na bei nafuu, hivyo nadhani wa Afrika wanacho cha kujivunia.

Swali ni kwamba je ni kweli TECNO watakuja na toleo jipya kama inavyosemekana midomoni mwa wadau mbali mbali, bado hakujakuwa na taarifa rasmi kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika

Mara nyingi TECNO inapohusishwa kuhusu toleo jipya bhaasi huwa kweli,je awamu hii TECNO wanakipi cha tofauti? Maswali yamekua mengi yakiacha wadau vinywa wazi wakiwa na shauku ya kutaka kuona ni nini TECNO watakachoingiza sokoni ikiwa ni muendelezo wa Camon.
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya http//www.tecno-mobile.com/tz

No comments: