Friday, March 30, 2018

WADAU WATARAJIA KITU TOFAUTI KUTOKA TECNO


Kufuatia ongezeko la matumizi ya simu za mkononi, makampuni mbali mbali yamekua yakija na matoleo tofauti ili kufanya vema sokoni,TECNO wakiwa ndo kampuni pendwa zaidi katika kuzalisha kile kinachomstahili mteja

Tayari pameshakua na minong’ono ya hapa na pale baina ya wadau wa simu janja “smart phone” ikiinyooshea vidole kampuni ya TECNO, kwa kuihusisha kampuni hiyo na ujio wa toleo jipya ambayo ni muendelezo wa Camon

Mbali na picha mbalimbali zilizozagaa mtandaoni zikionesha muonekano tofauti wa simu hiyo mpya kuzinduliwa, tayari kurasa za mitandaoni zimezua mijadala inayokosa majibu sahihi kuhusiana na simu hiyo, baadhi wakiifananisha simu hiyo mpya kutoka TECNO na zile za kampuni ya Samsung na Apple.



Wadau wamekua na shauku ya kutaka kujua ni kitu gani cha tofauti ambacho TECNO wameweza kukiongeza kwenye toleo hilo jipya

Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya http//www.tecno-mobile.com/tz

No comments: