Tuesday, April 10, 2018

NDANI YA MIEZI TISA TRA YAKUSANYA ZAIDI YA TRILIONI 10.


Katika kipindi cha miezi tisa ya mwaka wa fedha 2017/2018 Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA imekusanya kiasi cha shilingi Trilion 11.78 ikilinganishwa na shilingi Trilion 10.86 ambazo zilikusanya kwa mwaka wa fedha 2016/17.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Bw. Richard Kayombo akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam.

Akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Huduma kwa Mlipa kodi wa TRA Bw. Richard Kayombo alisema kuwa ongezeko hilo ni sawa na ukuaji wa pato kwa asilimia 8.46

Aidha Mkurugenzi huyo alisema kuwa katika kipindi cha mwezi machi peke yake TRA imekusanya jumla ya shilingi Trilion I.54, ikilinganishwa na makusanyo ya mwezi machi 2017 ambapo ilikusanya jumla ya shilingi Trilion 1.34 ambapo ni ukuaji wa asilimia 14.49.

Kayombo aliendelea kusema kuwa mafanikio yote haya yanatokana na juhudi za walipa kodi, viongozi wa ngazi zote na kampeni kadhaa, pamoja walipa kodi wapya nchi nzima kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati na kusikiliza malalamiko yao pamoja na kuwajengea utaratibu mzuri wa kulipa madeni yao ya nyuma.
Mkutano ukiendelea.

"Katika kipindi hiki tunaendelea na usajili wa walipa kodi wapya wakiwemo wamachinga ambapo kwa wiki hii tupo mkoani Geita, na tunawakaribisha wafanyabiashara wote wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi na kupewa namba ya utambulisho ya mlipa kodi(TIN) na maafisa wa TRA watasikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi" alisema Kayombo


Na mwisho Mkurugenzi huyo alisema kuwa katika kuhakikisha huduma zinazotolewa ni bora, TRA inaendelea kutoa elimu kwa kila anayestahili alipe kodi kwa hiari na kwa wakati na mwenye malalamiko yoyote juu ya makadirio amuone meneja wa eneo husika akiwa na vielelezo vyake vyote.

No comments: