Sunday, April 22, 2018

QNET IMEWAPONGEZA CAF NA KLABU ZA MPIRA WA MIGUU ZA AFRIKA KWA MAFANIKIO YAO KATIKA MASHINDANO YA MPIRA YA CAF MWAKA 2018

                                                                                              
Kampuni inayoongoza ya mauzo ya moja kwa  moja QNET, na mbia katika ligi ya mabingwa ya CAF, Kombe la Shirikisho la CAF na kombe la Super Cup imewapongeza Shirikisho la Soka Afrika, CAF na vilabu vyote vinavyoshiriki katika mashindano yote ya klabu ya CAF mwaka 2019.

QNEt imekaribisha ushirikiano wake na CAF, katika mwaka 2018 na inaelezea fahari yake katika mpira wa miguu wa Afrika.

Ushirikiano kati ya kampuni ya QNET na CAF ni sehemu ya juhudi za QNET za kukuza michezo Afrika na dunia kote.
Kwa kweli, kama ilivyo katika michezo, QNET inaongozwa na ari ya kufanya kazi kwa pamoja kama timu pamoja na shauku wakati inapofanya biashara zake kila siku.

Ushirikiano huu ni fursa nyingine kwa QNET kuwa karibu na wawakilishi wake wa kujitegemea (IRs), walaji na wateja ambako QNET inaendesha shughuli zake tangu zaidi ya muongo mmoja iliopita.

Meneja Mkuu wa QNET wa Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara, Biram Fall amesema kwamba, “Mwaka uliopita ulikuwa ni mwaka mzuri kwa mpira wa miguu barani Afrika. Katika QNET tunaona fahari sana kujihusisha na CAF na ukuaji wa mchezo wa mpira wa miguu barani. Falsafa ya biashara yetu inashikilia mwenendo wa mpira wa miguu, ambao kimsingi ni ufanyaji wa kazi katika timu, ushirikiano, shauku na kufanyakazi kwa bidii. Tunawawezesha wajasiriamali katika bara zima la Afrika na tumejikita katika kusaidia wengi zaidi waweze kufanikiwa. Vilevile ni heshima kwetu kudhamini mashindano haya maarufu na yanayoheshimiwa sana, na tusingeweza kupata mshirika bora zaidi kuliko Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) kuweza kufanikisha lengo hili. Mwaka 2019 unaonekana kutia matumaini zaidi na QNET itakuwa katika upande wa CAF kwaajili ya kuhakikisha utendaji bora zaidi”.

Katika mwaka 2019, QNET itakuwepo zaidi viwanjani ikiwa na uhamasishaji, matukio zaidi kwaajili ya kuhamasisha mashabiki kuongeza nguvu kazi ya mauzo ya QNET na wawakilishi wa kujitegemea (IRs).

QNET inaendelea kuongeza uwepo wake katika bara zima la Afrika, ikiwa inatoa fursa za ujasiriamali kwa watu na kusaidia watu kubadili historia zao vyema zaidi. Ukiachilia mbali ushirikiano wa kimichezo, QNET pia ni kampuni ambayo inajihusisha na majukumu ya kijamii, kutoa kwaajili ya maendeleo endelevu ya jamii katika kanda zote ambako inaendesha shughuli zake. Katika mwezi Novemba, kampuni ya QNET ilitunikiwa tuzo ya mwaka ya e-commerce CSD Company na Kituo cha Uwajibikaji kwa Jamii cha Afrika Magharibi (Centre for Corporate Social Responsibility West Africa)
   

1 comment:

parisafaas said...

Casinos near me - MapyRO
Find 전라북도 출장샵 Casinos near 아산 출장샵 me near you from 4020 Casinos in The 통영 출장샵 United States, with locations in Nevada, New 밀양 출장안마 Jersey 경상남도 출장안마 and Pennsylvania, and more.