Sunday, June 19, 2022

Efm kuzindua kipindi kipya kiitwacho "Jioni ya Leo"

Vipindi vingi vya redio vinavyoanza majira ya jioni kuanzia saa 10 havifanyi vizuri kama inavyotakiwa na hii nimeiona katika utafiti wangu na kuamua kuja na kipindi kitakachokonga nyoyo za mashabiki wetu hapa nchini Tanzania.

Hayo yameelezwa mapema jana mkoani Dar es salaam na Mkuu wa vipindi kutoka kituo cha Efm Redio Bw. Dickson Ponera wakati wa uzinduzi wa kipindi kipya kiitwacho "Jioni ya Leo" kitakachorushwa na Redio hiyo.

Aidha ameongeza kuwa kipindi hicho kitakuja kuleta mapinduzi makubwa sana kwani kitakuwa kimesheheni mambo mengi mazuri na kuunganisha watangazaji kutoka katika vipindi tofauti vya Efm, akiwemo Dina Marious aliyetoka katika kipindi cha uhondo, Osca Osca sports HQ, Mpoki na Roman Shirika kutoka kipindi cha ubaoni.

Ameendelea kusema kusema kuwa Kipindi hichi cha "Jioni ya Leo" kitakuwa siki za katikati ya wiki na kitaanza saa 10 mpaka saa 1 kamili usiku na kuchukua nafasi ya kipindi cha Ubaoni ambaho ndio kilikuwa kikianza na kumalizika muda huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Efm Bw. Dennis Busolwa (Sebo) akiongea na waandishi wa habari katika Tafrija fupi ya kutambulisha kipindi kipya cha "Jioni ya leo" kilichozinduliwa makao Makuu ya Media hiyo Mkoani Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Vipindi Efm Dickson Ponera (Dizzo ONE) akizungumza katika hafla iliyoandaliwa na kituo cha Radio cha Efm mapema jana mkoani Dar es salaam.
Mtangazaji wa Muda mrefu Dina Marios Akiongea na waandishi wa habari katika hafra fupi ya kutambulisha kipindi kipya cha "Jioni ya leo" kilichozinduliwa jana makao makuu ya Efm Redio Mbezi Beach mkoani Dar es salaam.
Tafrija ikiendelea.
Baadhi ya Viongozi na Watangazaji wa Efm wakishangaa bango la kipindi kipya cha "Jioni ya leo" baada ya uzinduzi mapema jana Mkoani Dar es salaam.




No comments: