Tuesday, August 16, 2022

Ripoti ya ya wafanyabishara wa Mipakani yazinduliwa leo jijini Dar es salaam.

Liberty sparks ni Shirika lisilo la Kiserikali, lilojikita katika elimu na tafiti, linalotekeleza mradi wa urahisi wa kufanya biashara nchini Tanzania ambao unafadhiliwa na taasisi ya Atlas Network”.

Mradi huu unategemea kuleta maboresho katika mazingira ya biashara kwa kutazama uboreshaji viashiria vya kiuchumi vinavyo tolewa na riport mbalimbali ikiwemo Ripoti ya Benki kuu ya dunia mwaka 2020. 

Mradi huu chini ya kampeni ya Ujirani mwema ,ambapo hapa tuna angaliautaratibu, muda na gharama katika utumaji na uingizaji wa bidhaa mipakani kwa kuzingatia muda,taratibu na gharama zilizowekwa kisheria.

Kama think tank, tumegundua sehemu ya biashara za mipakani kwa sasa Tanzania imekuwa haifanyi vizuri sana ukilinganisha na nchi nyingine zilizopo chini ya Jangwa la Sahara kama Mauritius, Rwanda, Kenya, Botswana, Burundi na nchi nyinginezo katika urahisi wa kufanya biashara.

Ingawa Tanzania ilipanda kwa ngazi tatu kwenye ripoti ya benki kuu ya dunia mwaka 2019 -2020 bado kuna huitaji mkubwa wa kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi, hili litatusaidia kutangaza na kuvutia wawekezaji nchini na kuwezesha vijana wetu kujiajiri wanapomaliza vyuo vikuu.

Naibu waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda Exaud Kigahe akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Wafanyabisahara wa Mipakani Mapema leo jijini Dar es salaam.

Liberty sparks inatambua mchango mkubwa wa serikali wa kuboresha mazingira rahisi na rafiki ya ufanyaji biashara pamoja na kutambua mchango mkubwa wa wadau katika kuchochea maendeleo ya nchi,na kutoa nafasi ya kufanya tathmini ya vipaumbele vya sera kwa kulinganisha na nchi na chumi zilizofanikiwa duniani kwa kuwa na mazingira bora ya ufanyaji biashara za mipakani na ukuaji wa uchumi katika kupambana na umaskini.

Katika kampeni hii tumefanikiwa kufanya tafiti ilayofanywa na Daktari Sauti Magai kutoka (College of Business) chuo kikuu cha Dar es Salaam. Tafiti hii inalenga kuboresha biashara za mipaka kama nilivyosema awali kwa kuzingatia taratibu,muda na gharama.

Sasa ili kufikia malengo hayo, tumeita wadau kutoka sekta binafsi pamoja na serikali na kuunda kikosi kazi kilichotoa mapendekezo ya pamoja kwa kuzingatia utendaji na uwakilishwaji wa moja kwa moja. 

Ni mategemeo yetu kupitia ripoti hii iliyotolewa leo na mgeni rasmi kuwa Mh Exaud Kigahe yataumika katika kufanya maboresho ya kisera na kuweka mazingira bora na rafiki yaufanyaji biashara Tanzania.

Tunaamini kwamba kila mtanzania akipata nafasi na kuweza kufanya biashara kwa urahisi, tutaweza kabisa kupunguza tatizo la umasikini na ajira kwenye kaya zetu kwa sehemu kubwa.

Hili litasaidia kuchochea maendeleo ya jumla na kuondokana na utegemezi. Hatua hii ya kuwaleta serikali na sekta binafsi kwa pamoja itasaidia kutoa mapendekezo yenye mchango chanya kwenye mpango wa muda mrefu wa Tanzania (TDV 2025), Mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2021/2022 - 2025/2026) na maendeleo endelevu ya Dunia 2030.

Wadau walioshiriki leo ni kutoka serikalini na sekta binafsi ni kama wafuatao; 

Ni matengemeo yetu Taasisi za kiserikali , waandishi wa habari, wabunge, wanazuoni na wadau wengieneo wa maendeleo watatuunga mkono katika kampeni hii ya kuboresha mazingira ya biashara Tanzania.

Matokeo ya mda mrefu na mfupi ya mradi huu ni kuona mazingira ya biashara yakichochea maendeleo ya nchi na watu kwa pamoja.

Baadhi ya Wajumbe wakufuatilia matukio yanayoendelea katika Uzinduzi wa ripoti ya Wafanyabiashara wa Mipakani.

1 comment:

Unknown said...

We had a great time! Let's private and government sectors to implement what been discussed!