Monday, February 25, 2013

SECTA YA KILIMO YAJIPANGA UPYA



Wizara ya kilimo,chakula na ushirika imepanga kuimarisha

Sekta ya kilimo nchini kwa kuzalisha vyakula vyenye lishe wakishilikiana na Agriculture Nutrition Capacity Development workshop (CAADP)

    Akizungumza jijini Dar es salaam waziri wa kilimo,chakula na ushirika .Eng CHRISTOPHER CHIIZA amesema mpango huu wa kuimrisha kilimo na lishe nchini utawasaidia wafanyakazi, watoto na wananchi kwa ujumla kupata vyakula vyenye lishe na ubora

        Aidha.Eng CHIIZA amesema kilimo ndio sekta ya uchumi tegemezi nchini  katika maisha yetu ya kijamii na asilimia 75 ya  watanzania hapa nchini ajira zao wanategemea katika kilimo

 

       Ameongeza kuwa katika mikoa ya hapa nchini ambayo ina uhaba wa chakula atahakikisha inapata chakula kutoka katika mikoa ambayo ina akiba ya chakula cha kujitosheleza na kuwataka wananchi wazalishe vyakula kwa wingi ili waweze kukabiliana balaa la njaa nchini.

 

        /YM         REPORTING

No comments: