Tuesday, February 26, 2013

WAZIRI MWINYI AZINDUA SHAHADA YA SAYANSI YA JAMII CHUO KIKUU HURIA

Waziri wa afya na usitawi wa jamii amezindua shaada ya masomo ya ustawi wa jamii katika chuo kikuu cha huria jijini Dar es salaam katika maadhimisho ya miaka 20 ya chuo hicho

 

Akizungumza katika  maadhimisho hayo waziri wa afya na ustawi wa jamii DR HUSSEIN MWINYI amesema serikali kwa kusaidiana na asasi za marekani watahakikisha wanawasaidia wanafunzi  wanao soma mitaara hii ili waweze kusaidia jamii ambazo watazitumikia

 

 

Aidha DR HUSSEIN MWINYI ameongeza kuwa kwa nchi  inayoendelea kama TANZANIA yenye matatizo ya kijamii kama ongezeko la umaskini,na tatizo la ajira nchini wafanyakazi wa jamii (social workers) ndio wanaweza wakawa suluhisho kwa mafunzo wanayopata

 

Nae vice chancellor Prof TOLLY S.A.MBWETTE amesema uwezo wa social workers Nchini TANZANIA utasaidia kuinua maisha ya watanzania kijamii na hata kiuchumi kwa ujumla

No comments: