Friday, March 1, 2013

WATEJA WA TIGO SASA WANAWEZA KUFANYA MALIPO KWA KUTUMIA MFUMO WA KIELETRONIKI WA MALIPO SERIKALINI (GePG)

Mkuu wa Huduma za Biashara na Serikali wa Tigo, Ally Maswanya (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mfumo wa Malipo ya Kieletroniki Serikalini (GePG) ambao utawezesha wananchi kulipia ankara mbali mbali za kiserikali kwa urahisi na moja kwa moja kwa njia ya simu za mkononi kupitia huduma ya Tigo Pesa. Pamoja naye ni Afisa Mwandamizi wa TEHAMA katika Wizara ya Fedha na Mipango, Bernard Mabagala (kushoto) na Mkuu wa Huduma za Tigo Pesa, Hussein Sayed (kati).

Fanya malipo ya haraka, urahisi na kwa usalama zaidi kwa zaidi ya idara 300 za serikali, mawakala na mamlaka za udhibiti kwa Tigo Pesa 

 Wateja wa Kampuni ya Tigo, sasa wanaweza kufanya malipo kutumia mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) baada ya kampuni hiyo kuongeza malipo ya Serikalini kwenye App yake ya Tigo Pesa.

Akiongea katika uzinduzi wa GePG kwa mtandao wa Tigo yaliyofanyika  jijini Dar es Salaam, Bernard Mabagala Afisa Mwandamizi wa TEHAMA – Wizara ya Fedha na Mipango alisema kuwa ubunifu na juhudi za Serikali katika  kuanzisha mdumo huo wa Kieletronbiki wa Malipo Serikalini (GePG) umerahisisha upatikanaji wa ankara na kufanya malipo kwa wananchi. Pia imeleta faida nyinginezo ikiwemo kuboresha uwekaji wa kumbukumbu, utoaji wa taarifa, kupunguza uvuvaji na ubadhirifu pamoja na kuongeza mapato kwa idara mbali mbali za Serikali. na

Baadhi ya wafanyakazi kutoka kampuni ya Tigo na Serikali wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya uzinduzi wa Mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Kupitia mfumo wa GePG Serikali pia imeongeza wigo wa upatikanaji wa huduma kwa wananchi na kuongeza fursa za biashara kwa kampuni zinazotoa huduma za malipo kama Tigo. Wananchi wanaweza kupokea ankara zao moja kwa moja kutoka ofisi na mashirika ya Serikali au kwa njia mbali mbali za kimtandao, na kufanya malipo ya ankara kwa urahisi na mahali popote kwa njia ya simu za kiganjani, benki au kwa njia ya mtandao. 

“Kufanya kazi kwa karibu na Serikali ili kufikisha huduma za kifedha kwa wananchi wengi ni moja kati ya malengo na mkakati wetu,” alisema Hussein Sayed, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za kifedha wa Tigo.

“Zaidi ya wateja milioni 7 wanaotumia huduma yetu ya Tigo Pesa sasa wana uwezo zaidi wa kufanya malipo kwa haraka kwenda kwa taasisi, Wizara na wakala wa Serikali zaidi ya 300 kupitia Tigo Pesa USSD, Tigo Pesa App na QR Code,” alisema Mkuu wa Kitengo cha Biashara na Serikali wa Tigo, Ally Maswanya.

Baadhi ya taasisi za Serikali ambazo malipo yanaweza kufanywa kwa Tigo Pesa ni pamoja na Wizara ya Ardhi, Shirika la Kodi Tanzania (TRA), Shirika la Umeme Tanzania TANESCO, Mamlaka za Miji, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Shirika la Hifadhi ya Mbuga za Taifa (TANAPA), Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mamlaka ya Misitu (TFS), Wizara Malia Asili na Utalii, Bodi ya Utalii, Idara ya Uhamiaji, Mamlaka za Maji katika miji ya Mwanza (MWAUWASA), Tanga (Tanga UWASA), Dar es Salaam (DAWASA), Dodoma (DUWASA), Hospitali mbali mbali kama vile Muhimbili, Mwananyamala na idara nyingine zaidi ya 300.

Ili kufanya malipo kwa kutumia Tigo Pesa App na QR Code, wateja wa Tigo wanahitaji kupakua App ya Tigo Pesa na kuscan QR code kisha kuingiza namba ya siri ili kufanikisha muamala.

Afisa Mwandamizi wa TEHAMA katika Wizara ya Fedha na Mipango, Bernard Mabagala (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mfumo wa Malipo ya Kieletroniki Serikalini (GePG) unaowezesha wananchi kulipia ankara mbali mbali SerikaliNI kwa urahisi na moja kwa moja kwa njia ya simu za mkononi kupitia huduma ya Tigo Pesa. Pamoja naye ni Mkuu wa Huduma za Tigo Pesa, Hussein Sayed (kati) na Mkuu wa Huduma za Biashara na Serikali wa Tigo, Ally Maswanya (kulia).



Ili kufanya malipo kwa kutumia menu ya Tigo Pesa, mteja anatakiwa kufuata hatua zifuatazo;.

1)      Kupiga *150*01# kisha kuchagua Lipa Bili
2)      Kuchagua namba 5 (Malipo ya Serikali)
3)      Kuingiza tarakimu 12 za mamlaka au taasisi anayotaka ipokee malipo
4)      Kuingiza kiasi cha fedha anachotaka kulipa
5)      Kuingiza namba ya siri kwa ajili ya kuruhusu malipo

Kwa upande mwingine, wateja wanaweza kutumia App ya Tigo Pesa ambayo inarahisisha ufanyaji wa malipo kwa kiasi kikubwa.

Baada ya kukamilisha malipo, wateja wa Tigo watapokea risiti ya kielektoniki kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi unaothibitisha kuwa muamala umefanyika kikamilifu. Risiti hiyo ya kielektroniki inakubalika kama uthibitisho tosha wa malipo na inaweza kusaidia kurahisisha kufuatilia malipo kwa kuwa ni rahisi kuhifadhi na kuipata pale inapohitajika ukilinganisha na risiti za karatasi ambazo ni rahisi kupotea au kuharibika.


Tigo inawakaribisha wateja wake kuanza kutumia huduma hii ya Malipo ya Kieletroniki Serikalini (GepG) sasa. 




No comments: