Wednesday, April 10, 2013

WANANCHI WA NGORONGORO WAAPA KUFIA KWENYE ARDHI YAO KULIKO KUMUACHIA MWEKEZAJI

 



Kiongozi wa Mila wa kabila la Wamasai Justin Nokoren  (kulia), akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, wakati viongozi wa mila na wananchi wa Ngorongoro  walipokuwa wakielezea mgogoro wao wa ardhi na Serikali katika Tarafa ya Loliondo, wilayani Ngorongoro. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Ololosolarm, Yannick Ndoinyo  wa Kata ya Arash, Mathew Silon.


Na Dotto Mwaibale

 

WANANCHI wa Wilaya ya Ngorongoro wameapa kufia katika ardhi ya wilaya hiyo badala ya kumuachia mwekezaji wa Kampuni ya Otterlo Business Corapation (OBC), kama serikali inavyotaka.

 

Hayo yalisemwa na Diwani wa Kata ya Olosokwani Yamick Ndoinyo wakati akizungumza na waandisghi wa habari Dar es Salaam jana huku akiwa na wajumbe wengine kutoka katika wilaya hiyo kuhusu mgogoro wa ardhi ya  Loliondo na kutoa maazimio kwa serikali.

 

"Kwa niaba ya wananchi wa Loliondo pamoja na viongozi wetu tunaitaka Serikali iache mara moja mpango wake wa kugawa ardhi ya vijiji vyetu kwa manufaa ya mwekezaji kwa kisingizio cha manufaa ya umma badala yake itambue ardhi yote ya Loliondo ni mali ya vijiji hivyo iviachie vijiji kujipangia matumizi yao ya ardhi kwa njia shirikishi na mujibu wa sheria za ardhi" alisema Ndoinyo.

 

Alisema serikali isipo badilisha msimamo wake wake wananchi wa Ngorongoro kwa umoja wao watalilinda ardhi hiyo kwa njia zozote zile kwani ndio uhai wao.

 

Ndoinyo aliendelea kutabainisha kuwa  serikali inatakiwa kuacha kupotosha umma kwamba ardhi hiyo siyo ya vijijni na ieshimu sheria kwa kuvipa vijiji haki yao ya kujiamulia mambo yao yenyewe kwa kutumia sheria zilizopo za ardhi na za serikali za mitaa.

 

Ndoinyo alisema serikali inatakiwa kuacha vitisho kwa wananchi wa Loliondo na wawakilishi wao, wanaharakati, mashirika na waandishi wa habari wanaoufatilia mgogoro huo.

 

Naye Diwani wa Kata ya Soistan Daniel Ngoitiko alisema serikali kuendelea kuyatisha makundim hayo inakiuka haki ya kikatiba ya kupata habari na kuzuia jamii kuelimishwa juu ya haki zao za kikatiba na kisheria kwa manufaa yao wenyewe na taifa kwa ujumla.

 

"Kuendelea kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya kupata taarifa na kutoa maoni kama inavyolindwa na katiba ya Tanzania na mikataba ya  Kimataifa ambayo serikali imeridhia" alisema Ngoitiko.

 

Maazimio hayo yamefikiwa na viongozi wa vijiji na  Kata za Ololosokwan, Malambo, Olorien. Soitsambu na Arash na vijiji vya Piyaya, Soitsambu, Oloirien, Arash, Malambo na Ololosokwan kwa niaba ya wenzao ambao hawakufika Dar es Salaam.

 

Mgogor huo umeibuka baada ya machi 21 mwaka huu Waziri wa Maliasikli na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kutoa taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari kuwa wizara hiyo inabadilisha mipaka na ukubwa wa eneo la pori tengefu la  Loliondo kutoka kilometa za mraba 4,000 hadi 1500.

 

Katika taarifa hiyo Waziri alitangazia umma kwamba Serikali imeamua kupunguza ukubwa wa eneo hilo ili kutatua migogoro iliyopo kataika eneo hilo, kunusuru ikolojia ya hifadhi ya Serengeti, Ngorongoro na Pori tengefu la Loliondo.

 

Mgogoro katika eneo hilo la Loliondo umedumu kwa muda mrefu na inaanzia mwaka 1992 wakati serikali ilipoingia katika mkataba na Kampuni ya Otterlo Business Corapation ya kutumia ardhi za vijiji bila ya kushirikisha vijiji na bila ridhaa yao

 

No comments: