Thursday, June 20, 2013

NUSU YA WATANZANIA HAWANA ELIMU YA UKIMWI--- TACAIDS



 
 Imeelezwa kuwa bado zaidi ya nusu ya watanzania wote hawana uelewa sahihi juu ya ugojwa wa ukimwi jambo ambalo  limetajwa kuwa ni  hatari katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo.
          Hayo yamesemwa leo jijini dar es salaam na mkurugenzi mtendaji wa tume ya kudhibiti ukimwi tanzania (TACAIDS) DK FATUMA MRISHO katika mkutano uliowakutanisha viongozi mbali mbali wa afika wanaoshiriki katika mapambano dhidi ya ukimwi kwa lengo la kuwasilisha taarifa inayohusu jitihada zinazofanywa na bunge la tanzania katika kupambana na ugonjwa huo
             Dk FATUMA amesema kuwa katika utafiti uliofanya na tume hiyo katika miko ya tanzania bara imeonyesha wazi kuwa bado uelewa wa maambukizi ya ukimwi hasa maambukizi mapya bado ni mdogo jambo ambalo bado linahitaji jitihada za ziada kutoka kwa wadau mablimbali
           Aidha amesema yapo maneno yanayoenezwa  watu kuwa elimu ya ukimwi imeenea tanzania nzima hivyo hakuna haja ya serikali kuwekeza nguvu nyingi tena katika kutoa elimu ya ugonjwa huo jambo ambalo amesema sio sahihi kwani bado elimu ya ukimwi inahitajika sana hasa vijijini ambako elimu hiyo haijafika vya kutosha.
             Katikia hatua nyingine amesema tanzania ndio nchi ambayo imefanikiwa sana katika kupambana na ugonjwa huo ambapo amesema kuwa zaidi ya asilimia 93 bado hawana maambukizi ya ukimwi
           Katika mkutano huo umehudhuriwa na maraisi wastaafu wa afrika akiwemo raisi wa awamu ya tatu wa tanzania mh BENJAMINI MKAPA pamoja na raisi mstaafu wa Botswana mh FESTUS MOGAE.

No comments: