Friday, June 21, 2013

SERIKALI KUONGEZA MAHAKAMA KUU SITA



 
          
      Jaji mkuu wa tanzania jaji OTHUMAN CHANDE amesema serikali  katika mwaka ujao wa fedha ipo katika mpango wa kuongeza mahakama kuu  nyingine sita katika mikoa ambayo haina mahakama kuu kwa lengo la kupunguza upungufu wa mahakama tanzania
         Kauli hiyo ameitoa leo katika sherehe za 48 za kuwakubalia na kuwasajili mawakili wapya 127 leo jijini dar es salaam,amesema kuwa pamoja na kuwaapisha mawakili hao bado tanzania ina upungufu mkubwa wa mawakili ambapo amesema tanzania nzima ina mawakili 3455 ambao amesema ni idadi ndogo ukilinganisha na mahitaji yaliyopo
         Aidha amesema kuwa mawakili waliosajiliwa leo waende kufanya kazi hasa maeneo ya vijijini tofauti na sasa ambapo asilimia 75 ya mawakili wote wapo jijini dare s salaam.
          Hata hivyo amesema kuwa moja ya mjukumu ya majaji hao ni kutenda haki kwa wananchi wote kama taaluma yao inavyohitaji hivyo amewaasa mawakili hao kuhakikisha wanazingatia hilo
            Katika hatua nyingine moja kati ya mawakili waliosajiliwa leo bi KONSOLATA MPEPO amesema wao kama majaji jukumu lao ni kuwasaidia wananchi katika maswala ya sheria hivyo amehidi kufanya kazi katika eneo lolote la tanzania

No comments: