Sunday, August 4, 2013

BREAKING NEWZZ,--NI MUGABE TENA

Zimbabwe's President Robert Mugabe addresses a media conference at State house in Harare, on the eve of the country's general elections, July 30, 2013. Heavily armed riot police deployed in potential election flashpoints in Zimbabwe on Tuesday on the eve of a poll showdown between Mugabe and Prime Minister Morgan Tsvangirai that remains too close to call. REUTERS/Philimon Bulawayo (ZIMBABWE - Tags: POLITICS ELECTIONS)

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameshinda uchaguzi wa rais, baada ya kupata asilimia 61.9 ya kura. Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai ni wa pili na asilimia 33.9 ya kura

         Kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai ameueleza uchaguzi huo kuwa ni wa bandia na udanganyifu mkubwa na chama chake cha Movement for Democratic Change (MDC) kimeapa kutokubali matokeo, hali inayozusha hofu ya kurejewa kwa ghasia zilizomwaga damu ambazo zilitokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2008.

       Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amezitaka pande zote mbili "kutoa ujumbe wa wazi wa utulivu" kwa wafuasi wao wakati hali ya wasi wasi ikiongezeka.

          Ban ana matumaini kuwa hali hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa shwari na ya amani katika siku ya uchaguzi , itaendelea wakati wa zoezi la kuhesabu kura na hata baada ya kukamilika zoezi hilo," amesema msemaji wa katibu mkuu Martin Nesirky.

            Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika SADC ambayo ina ushawishi mkubwa pia imewataka "Wazimbabwe wote kuwa na uvumilivu,na utulivu."

Macho yote sasa yanaelekezwa kwa chama cha MDC ambacho kilitarajiwa kutoa taarifa yake leo Jumamosi(03.08.2013) kufuatia mkutano wao wa siku mbili.

      Kabla ya mkutano huo , afisa wa ngazi ya juu wa MDC Roy Bennett alitoa wito wa kampeni ya upinzani wa chini kwa chini, akiwataka watu "kuifikisha nchi hiyo katika hali ya kutoweza kufanya lolote".


No comments: