Friday, November 15, 2013

WADAU WA ELIMU WAENDELEA KUMKALIA KOONI PINDA,SASA APEWA SIKU SABA AWEKE WAZI RIPOTI YA TUME ALIYOUNDA KUCHUNGUZA MATOKEO MABAYA YA KIDATO CHA NNE



MKURUGENZI WA MTANDAO WA WANAFUNZI TANZANIA TSNP ALPHONCE LUSAKU AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

             MTANDAO wa Wanafunzi nchini “TSNP’ umemtaka Waziri mkuu nchini , Mh Mizengo Pinda kuitoa hadharani mara moja Ripoti ya tume iliyoundwa kwa ajiri ya kuchunguza matokea ya kidato cha nne,
      
         Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi  wa mtandao huo wa wanafunzi nchini, ALPHONCE LUSAKU amesema  wao Umoja wanafunzi wanamuomba waziri mkuu atoe ripoti ya tume hadharani ili wananchi wafahamu,

      
       “Tunamtaka wazir mkuu Mh Mizengo Pinda. Ndani ya wiki moja, atoe Ripoti ya tume  hadharani.Juu ya madhaifu yaliyopatikana,wakina  nani wamehusika na madhaifu husika,mapendekezo ya tume husika ili yasijurudie tena  kwa wadogo zetu’”alisema LUSAKU

      
         Vilevile mtandao huo wa wanafunzi  nchini wamemtaka pia mwenyekiti wa tume hiyo pia ambaye ni katibu wa Wizara ya elimu kwa sasa Profesa Sifuni Mchome ajitokeze hatokeze Hadharani na aitoe ripoti husika kwa watanzaia.

         
       Ripoti hii iliundwa baada ya matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka jana,yalionyesha kuwa watainiwa walikuwa 397,136  kati ya wanafunzi hao nusu yake walipata daraja la sifuri,na kupelekea kuwepo kwa manunguniko mengi kutoka kwa wadau wa elimu pamoja na wananchi,

     
        Kwa upande mwingine mwenyekiti mtandao huo wa wanafunzi nchini Julias Maila alimtaka waziri wa elimu nchini, Shukuru kawambwa kusitisha mala moja mabadiriko ya madaraja ya kwawanafunzi wa kidato cha nne


       “Tumesikitishwa sana na mkanganyiko uliojitokeza hivi karibuni,juu ya uwepo wa division “o” na division ‘5” kati ya katibu wa wizara mkuu wa wizara ya elimu  profesa Sifuni Mchome na Naibu waziri wa elimu Mhm Philipo Mlugo .Hasa katika wakati huu anbapo wadogo zetu wa kidato cha nne wanafanya mitihani yao ya mwisho”alisema Maila    


        Katika Hatua nyingine Umoja huo wa wanafunzi wamefika maamuzi, endapo waziri mkuu Mizengo Pinda hatatoa ripoti ya tume hiyo ndani ya wiki moja,watachukua jukumu la la kuwaunganisha wanafunzi wa vyuo vikuu nchini,wanafunzi wa sekondari na shule za msingi nchini,wadau mbalimbali wa elimu,vyama vya siasa,wazazi na watanzania kwa ujumla wake watafanya njia kwa ajili ya kuinusuru elimu nchini.    


No comments: