Wednesday, January 29, 2014

BREAKING NEWZZ----HAWA NDIO VIONGOZI WA CCM WANAOTAJWA KUANZISHA CCJ,MWENYEKITI WAO AWATAJA LIVE,ASEMA WANA KADI MBILI WARUDISHE MARA MOJA

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA CHAMA CHA JAMII CCJ BW RICHARD KIYABO AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

        Mwanzilishi wa chama cha kisiasa cha CCJ ambaye kwa sasa amekikimbia chama chake na kujiunga na chama cha mapinduzi CCM leo ametoa kali ya mwaka baada ya kuitaka CCM iwape adhabu wanachama wake ambao wanamiliki kadi mbili yani ya CCJ na CCM huku akiwataja kwa majina
       
        Bw RICHARD KIYABO ambaye ndiye aliyeanzisha chama cha CCJ leo amejitokeza mbela ya wanahabari jijini dar es salaam na kusema kuwa amemwandikia barua makamu mwenyekiti wa ccm mh PHILIPO MANGULA akimtaka achukue hatua kali kwa wanachama wake ambao sio waadilifu kwa chama chake na wamekisaliti chama chao na kwenda kuanzisha CCJ kwa lengo la kukiua CCM
  
         “nashangaa ndani ya chama bado kuna wanacham na viongozi waandamizi wana kadi mbili yani ya CCM na CCJ na wameshindwa hadi sasa kuzirudisha na kuomba radhi kwa wanachama kwa usaliti huo”alisema bw KIYABO.



MAJINA YA MICHANGO YA CCJ YA KUANDAA MAANDAMANO AMBAYO VIONGOZI WA CCM NAO WANATAJWA KUCHANGIA
           Bw KIYABO pia aliayaambatanisha majina ya wanachama wa ccm waliowahi kushiriki katika kuchanga hela kwa ajili ya kukisaidia chama cha CCJ kufanya maandamano ya amani nchi nzima huku orodha hiyo akiwa na majina ya viongozi wakubwa wa CCM kama mwakyembe, samweli sitta nape,anna kilango na wenginme wengi

No comments: