Wednesday, January 29, 2014

KAZI 907 KUSHINDANISHWA KATIKA TUZO ZA WAANDISHI ZA AJAT MWAKA HUU

KATIBU MTENDAJI WA BARAZA LA HABARI TANZANIA MCT AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI LEO JIJINI DAR ES SALAAM
Braza la habari Tanzania MCT limetangaza kupokea jumla ya kazi 907 za waandishi wa habari ambazo zitashindaniwa katika tuzo za waandishi wa habari zitakazofanyika mwaka huu katika ukumbi wa mlimani city march 14
Akizungumza na wandishi wa habari leo jijini dar es salaam katibu mtendaji wa baraza hilo bw KAJUBI MUKAJANGA amesema kuwa idadi hiyo ni pungufu kidogo ya kazi zilizopelekwa mwaka jana ambapo kazi 946 zilikusanywa.
Amesema kuwa katika waandishi waliioongoza kupeleka kazi nyingi bado wanatoka makampuni ya mwananchi communication kama ilivyokuwa mwaka jana,huku akisisitiza waandishi kujifunza kushiriki katika tuzo hizo kwani zitaajengea uzoefu mkubwa.
Washindi wa tuzo hizo watakabidhia zawadi zao katika usiku wa march 14 mwaka huu katika ukumbi wa mlimani city ambapo mgenirasmi anatarajiwa kuwa raisi wa mahakama yay a jumuiya ya Africa mashariki mh jaji HAROLD NSEKELA

No comments: