Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Anne S. Makinda (Mb), anasikitika kutoa taarifa ya
kifo cha Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe. Saidi Ramadhani Bwanamdogo
Kilichotokea leo Jumatano asubuhi tarehe 22.1.2014 Katika
hospitali ya MOI DSM alipokuwa amelazwa kwa Matibabu.
Ofisi inaendelea na taratibu za mazishi kwa
kushirikiana na familia ya Marehemu.
Inna llilah Waina Illaih Rajiun!
SPIKA WA BUNGE,
22.01.2014.
|
No comments:
Post a Comment