Naibu
Waziri wa Wizara ya Fedha, Mwigulu Nchemba, ambaye alikuwa miongozi mwa
manaibu waziri walioapishwa na Rais Jakaya Kikwete kushika nyadhifa zao
amewaambia watu wanaoponda uteuzi wake kuwa hana haja ya kubishana nao kwani
hawamjui.
Katika maelezo yake, Mwigulu alisema anamshukuru Mheshimiwa
Rais kwa kumwamini kuwa anaweza kumsaidia katika kusimamaia sera na mipango ya
fedha nchini. Watu wasionifahamu wanadai mimi sina viwango vya kufanya kazi
hii; naomba wafahamu kuwa mimi ni msomi mwenye shahada ya ya pili ya uchumi na
hivi sasa niko katika masomo ya kupata shahada ya uzamivu.
Mwigulu
aliendelea kusema “Kabla sijaingia kwenye siasa nilikuwa nafanya kazi katika
Benki Kuu ya Tanzania kama mchumi. Ninakwenda Wizara ya Fedha kusimamia mambo
manne ambayo ni uadilifu, ushirikiano, jitihada na huduma madhubuti ambazo
zitatolewa kwa wakati mwafaka.
No comments:
Post a Comment