Saturday, January 18, 2014

MBOWE AIBUKIA KWENYE UCHAGUZI WA NCCR,ATOA YA MOYONI,AHOFIA CHADEMA KUPASUKA KAMA NCCR-MAGEUZI,SOMA YOTE ALIYOYASEMA



 
Na Karoli Vinsent
       
       MWENYEKITI wa chama cha democrasia na Maendeleo’ CHADEMA Freeman Mbowe ,amehofia chama chake huwenda kikapata mpasuko,kama uliowakuta Chama cha NCCR Mageuzi kipindi cha nyuma.
      
    Hofu hiyo ilibainika Leo wakati wa Mkutano mkuu wa Chama cha NCCR Mageuzi uliofanyika jijin Dar es Salaam,ambapo Freeman Mbowe alipokuwa anazungumza kwa niaba ya Vyama vya upinzani,alisema watu wengi hawajui historia ya vyama vya kisiasa vilivyoanzia ,

  “Leo watu wengi hawajui vyama hivi vya kisiasa vimeanzia wapi kwa mfano chama cha NCCR  kimepitia sehemu nyingi hebu tukumbuke wote chama hiki kipindi kile walipoibuka “UDETA” Umoja wa Demokrasia Tanzania walibuka watu wakawa wakaipasua chama hichi, wako wanaojiita NCCR asilia,leo wako wapi na kila chama cha upinzani Tanzania kitapia Sehemu hii hata  mimi napitia huku”alisema Mbowe  
      
    Freemani Mbowe ambaye ni Mbunge wa Jimbo Hai kupitia Chama  Cha Chadema na pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzania Bungeni alizidi kusema kuwa inahitajika nguvu kubwa sana  kuvilinda vyama vya kisiasa
  
    “Kukiua Chama cha Kisiasa ni kazi ndogo sana ila Kukijenga chama cha Kisiasa ni kazi kubwa ambayo inaitaji  hata kipindi cha muongo mmoja mpaka kukirudisha chama hicho,tunaitaji nguvu kubwa sana kuvilinda vyama ,leo tunaitaji Nccr au Cuf,Chadema yenye nguvu tuweze kuijenga nchi na tuweze kuondoa CCM mdarakani”alizidi kusema Mbowe
            

                  KUHUSU KATIBA MPYA-ENDELEA HAPO------

       
        Mwenyekiti  huyo wa Chadema aliwataka vyama vya kisiasa visiingilie katika mchakato huu wa katiba Mpya kwani wanaweza kuharibu mwenendo huu wakatiba mpya
        
      “Leo nashangaa sana sisi wanasiasa tunavyoingila mchakato huu wa katiba mpya nashangaa sana leo CCM wanavyosema  wao wanaunga mkono serikali mbili kwakuwa sio ilani ya chama  chao, swali la kujiuliza je katiba hii ni ya chama au ya wananchi, nawaomba wanasiasa wenzangu tusiingilie mchakato huu kwani tutakuwa tunahalibu kwani katiba hii si ya wanasiasa bali ya wananchi hata wengine wasiokuwa na chama”alimalizia  Mbowe
      
         Kwa upande wake Kada wa  Chama cha Mapinduzi CCM Mustafa Jaffer Sabodo alivitaka vyama vya kisiasa nchini hususani chama cha Wanchi CUF pamoja na Chadema na Chama cha NCCR mageuzi kuungana ili waweze kuingoa CCM madarakani,

    “Naviomba vyama CUF na NCCR pamoja na CUF unganeni ili muweze kuingoa CCM madarakani,nataka niwambia kuwa kuiondoa CCM mdarakani inahitajika nguvu kubwa sana kutoka kwenye vyama hivi”alisema Sabodo

    Katika hatua nyingine Kada huyo wa Chama cha Mapinduzi akatoa hundi yenye Thamani ya Sh milioni 20 kwenda kwa Chama hicho cha NCCR pamoja na kukihaidi chama hicho kukipia msaaada kwenye Majimbo ya Wabunge wachama hicho Maendeleo ikiwa ni pamoja na kuwajengea visima  vya maji kila Jimbo
      
        Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM “bara”  Philipo Mangula alikipongeza chama cha NCCR kwa kazi kubwa walioifanya sana mpaka kufika Chama hicho kufanya Mkutano huo mkuu
       
      Mpaka Mwandishi wa mtandao huu anaondoka ukumbini hapo Chama hicho cha siasa kulikuwa bado akijanza kufanya uchaguzi mkuu wa chama hicho

No comments: