Tuesday, April 1, 2014

NHC WATOA PUNGUZO LA ASILIMIA SITA,NI KWA WALE WATEJA WA KWANZA,NYUMBA ZIKO HUKO HANANASIFU KINONDONI

Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), David Shambwe, akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi mpya za shirika hilo zilizopo jijini Dar es Salaam leo, kuhusu uuzwaji wa nyumba za shirika hilo katika mradi wa Eco Residence zilizopo Kinondoni Hananasif Dar es Salaam.(kushoto) ni Meneja Mauzo wa Shirika hilo Tuntufye Mwambusi na Kulia ni Meneja Huduma za Jamii wa NHC, Muungano Saguya.

 
Mchoro wa namna litakavyokuwa jengo la Eco Residence litakaloanza kujengwa katika kitalu namba 67 kwenye makutano ya mitaa ya Ngano na Wakulima, Dar es Salaam litakapokamilika litakuwa na ghorofa 16, sehemu za makazi 118 na kuwa makazi ya watu zaidi ya 840 wakati kabla lilikuwa makazi ya familia moja.

 Ujenzi wa jengo hilo uliovpofikia kwa sasa
Hii hapa ndiyo Timu ya mauzo ya Shirika la Nyumba la Taifa ikiwa katika eneo hilo, wahi sasa upate punguzo lako la bei
 
 Mhandisi Anna Mrema wa kampuni ya ujenzi wa Estim Construction Ltd inayojenga jengo hilo la makazi akiwa anazungumza na vyombo vya habari asubuhi hii kuhusiana na ujenzi wa jengo hilo
Eneo la Ujenzi mtaa wa Ngano na Wakulima
 
 Ujenzi wa jengo hilo uliovpofikia kwa sasa

Timu ya NHC pamoja na wakandarasi wa mradi huo wa wakulima

HII HAPA TAARIFA KAMILI JUU YA MRADI HUO

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UUZWAJI WA NYUMBA ZA ECO RESIDENCES, DAR ES SALAAM


Kwa mara nyingine tena leo Jumanne ya tarehe 1, Aprili, 2014, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linayo furaha ya kuwatangazia rasmi Watanzania wote mauzo ya sehemu za nyumba za makazi (units) 118  za mradi ujulikanao kama Eco Residence, uliopo katika eneo tulivu la Hananasif – Kinondoni, Dar es Salaam. 

Nyumba  hizo za gharama ya kati na juu zipo Kilomita 6 kutoka katikati ya jiji la Dar es salaam, zikiwa karibu kabisa na maeneo ya Oysterbay, Upanga na Masaki.

Tungependa kuwajulisha watanzania kuwa uzinduzi wa mauzo ya sehemu ya nyumba hizi hii leo unawapa tena fursa ya kujiandaa kwa zaidi ya wiki tatu ambapo mauzo rasmi yataanza  tarehe 23 Aprili, 2014.

Hivyo, tunawakaribisha  watanzania wenye nia ya kununua nyumba za mradi huo kuwa ifikapo tarehe hiyo waanze kulipia  asilimia kumi kama malipo ya awali na baadaye wamalizie malipo yao kupitia mikopo kutoka kwenye benki washirika 12  ambazo NHC imeingia makubaliano nazo. Kwa kufanya hivyo watanzania hao wataweza kupata fursa ya kuwa wamiliki wa nyumba hizo bora na za kisasa kabisa zinazojengwa na Shirika katika eneo lenye ardhi yenye thamani kubwa.

Nyumba hizi tunazotangaza hii leo ziko za aina na ukubwa mbalimbali  zinazolenga kukidhi mahitaji ya wananchi mbalimbali wenye uwezo wa kulipa kuanzia kiasi cha shilingi millioni  199  mpaka million 253 bila VAT ili kuwawezesha kila mwananchi kuwa na uchaguzi mpana kulingana na uwezo wake. Kwa wanunuzi wataonunua nyumba ndani ya siku tisini watapata punguzo la asilimia 6.

Nyumba za Eco Residence zina vyumba vitatu chumba kimoja kikiwa kimejitosheleza na kuna huduma zote muhimu. Tunawahamasisha na kuwakaribisha watanzania wote walio nchini na walio nje ya nchi wafanye mawasiliano na Makao Makuu ya Shirika, Ofisi zetu za Mikoa au kupitia baruapepe na kukamilisha taratibu mapema kwa ajili ya kuweza kuingia kwenye mchakato ulio wazi wa manunuzi.

Ukiwa mdau na mnunuzi mtarajiwa ama una ndugu/rafiki anayetamani kununua nyumba katika mradi huu, tafadhali waweza kuwasiliana na  Kitengo cha Mauzo simu namba 0754 444 333; baruapepe: sales@nhctz.com na pia tembelea tovuti ya Shirika www.nhctz.com  au Ofisi za NHC zilizoko mikoa yote Tanzania kwa maelezo zaidi.
Mauzo ya Nyumba hizi yanafanywa na Shirika la Nyumba la Taifa peke yake, hakuna dalali au wakala yeyote anayehusika au atakayehusika na mauzo ya nyumba hizo.SHUKRANI FULLHABARI BLOG

No comments: