Monday, May 19, 2014

AHADI FEKI--NAPE NNAUYE WA CCM AMTAPELI MSHINDI WA MAISHA PLUS 2012,MWENYEWE AKANA KUHUSIKA.SOMA HAPA

Na Karoli Vinsent
           
       CHAMA cha Mapinduzi CCM,kimeingia kwenye Kasfa Kubwa kutokana na Chama hicho kufanya Utapeli wa ahadi ambao umemkumba Katibu Mwenezi Itikadi wa Chama Cha  (CCM) Nape Moses Nnauye baada ya kutoa ahadi kwa mshiriki wa shindano la Maisha Plus Bernick Mathias Kimiro wa mwaka 2012.

Utapeli, huo umethibitika jana siku ya jumapili katika sherehe za kumtangaza mshindi wa Maisha Plus/Mama Shujaa mwaka 2014, ambapo aliekuwa MC wa shughuli hiyo  Masoud Kipanya alipomuomba Bernick Kimiro ambae ni mshindi aliepita ainuke kutoa neno kabala ya kukabidhi taji kwa mshindi mpya.

      Aidha, baada ya kutoa shukrani zake na kumpongeza mshindi wa mwaka 2014 ambae ni Boniphace Meng'anyi Nyakena kutoka Dar es salaam, Kimiro alisema “ Naomba nitoe ya moyoni, Mheshimiwa nape alikuja kijijini akaahidi kwamba kwaniaba ya chama cha mapinduzi kuwa watatoa nusu ya zawadi kwa kijana atakaye kuwa mshindi wa maisha plus kwa mwaka 2012”


“na mimi ndiye niliyekuwa mshindi kwa mwaka huo baada ya maisha plus kukamilika  hakunipa zawadi zangu, wao wakajaribu kunisaidia kumfatilia Nape wakaona anawasumbua wakaamua kulirudisha hilo swala kwangu” alisitiza Kimaro.

Aidha Kimaro aliasema hayo akiwa anarekodiwa na kurushwa moja kwa moja na televiheni ya Taifa TBC1, kutoka katika kijiji cha REKEBISHA kulikofanikia shughuli hizo, za kuwapata washindi hao ambao ni vijana na kina mama kwa upande wa mama Shujaa.

Mshindi huyo alipata zawadi ya shilingi milioni 20, kutoka kwa Maisha Plus ambapo kwa mujibu wa Nape alipotangaza atatoa nusu ya gharama takazo pewa mshindi kwa niaba ya chama hivyo ni sawa na ahadi ya shilingi milioni 10 taslim ambayo ndio nusu ya gharama zilizo tolewa na waendeshaji wa mashindano hayo.

Akiongea kwa masikitiko Kimaro alieleza “nilienda mwenyewe ofisi za chama wakanipa namba ya Nape nikampigia nikajieleza akaniambia nisubiri atanipigia lakini hakufanya hivyo, nikaendelea kumtafuta kwa ujumbe mfupi wa simu (SMS) pamoja na kupiga simu lakini sikufanikiwa kumpata wala kuongea Naye tena na mwisho namba ikawa haipatikani.

Baadae nikaamua kumfatilia ofisini kwake lakini nikawa napewa majibu kuwa nisubiri hayupo ijapokuwa nilikua naonyeshwa gari lake kwamba yupo ndani nikaambiwa nifate itifaki (protocol) kwa kuandika barua nikafanya hivyo kama mara tatu bila mafanikio.

nikaomba msaada kwa Kada mmoja wa chama akanipeleka kwa mheshimiwa Kingunge Kumbaremwiru  nikamweleza suala langu akaniambia hamna shida kwasababu ahadi ilitolewa kwa niaba ya chama nitapewa akawasiliana na Katibu wa Chama Abdurahmani Kinana likini pia hapakuwa na mafanikio.

Nikapelekwa kwa mbunge Wangu wa kinondoni Iddi Azan nae akaniahidi atafatilia lakini mwisho wa siku nikaachwa njia panda kwani sikupata msaada wowote mpaka sasa na kama unavyojua ahadi ni deni nakiomba chama cha mapinduzi wanipatie hiyo fedha kwani waliahidi wenyewe mbona Nyarando alitimiza ahadi zake sasa kwa  Nape inakuaje?????? Alisistiza Kimaro.

Aidha suala hilo liliwaacha midomo wazi na kufanya wageni waalikwa wengine kushindwa kutoa ahadi zao walipopanda jukwaani, na kuishia kuwaita viongozi wa Maisha Plus/Mama Shujaa waende ofisini kwao ili wakaongee jinsi ya kushirikiana nao.

Kati ya waliotoa mialiko wa aina hiyo ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Yamungu Kuyandabila ambae alikuwa ni mgeni rasmi wa sherehe hizo.

Aidha kwa upanda wa baadhi ya wageni waalikwa walisikitishwa sana na kitendo hicho cha kiongozi wa chama tawala kushindwa kutekeleza ahadi alizoahidi kwa kijana huyo huku wakidai kuwa wao wanamipango mizuri kwa maendeleo ya vijana.

Akizungumza kwa masikitiko, mgeni moja ambae alijitambulisha kuwa yeye ni kiongozi wa vijana wa chama hicho ambae  hakutaka kutajwa jina alisema” Nimepokea habari hizi kwa huzuni kubwa na inaonesha ni jinsi gani chama changu kinashindwa kutekeleza sera zake kwa jamii, kama chama kimeshindwa ahadi ya milioni 10 itawezekana ahadi ya kuliondoa taifa katika janga la umaskini? Alijiuliza mchangiaji.

Pamoja, na hayo mshindi mwingine ambae alijichukulia fedha taslimu shilingi milioni 25 kutoka Oxfan ni Mama Shujaa Bahati Muriga mwalimu mkuu shule ya msingi Muhozya Mwanza ambae pia ni mjasiria mali anaefanya kilimo cha chakula.

Mwandishi wa Mtandao huu ulimtafuta Katibu Mwenezi Itikadi wa Chama Cha Mapinduzi, (CCM) Nape Moses Nnaueye kutaka kujua Hatma ya Mshiriki huyo,pamoja na Ahadi hiyo,ambapo Nape alikana kuwa mgeni Rasmi kwenye Michuano hiyo.

“Sikiliza Mwandishi,Sijawai kwenda kwenye Mashindano hayo ya Maisha Plus,na Sijawai kumwahidi mtu na Kutotimiza Ni Ahadi vizuri mkamtafuta Muandaaji wa Mashindani Masoud kipanya”

“Na hilo nasikia kutoka kwenu na nimeona kwenye Mitandao ya kijamii,kwamba nimewai kutoa ahadi yeyote, kiukweli sijatoa ahadi yeyote na vilevile kushiriki au kuwa Mgeni Rasmi,na hizo Ni Habari za kutungwa na kunichafua mimi”alisema Nape.

Nape,ambaye anatoka kwenye Chama Kikongwe Afrika ambacho kipo Madarakani,alizidi kusema chama hicho hakina mpango wa kutoa ahadi za uongo na Kumtaka Mwandishi wa Mtandao huu amtafute Mwandaaji ya Mashindano Masoud Kipanya amuulize  kama Nape aliwai kuwa Mgeni Rasmi.



Mwandishi wa Mtandao huu alimtafuta Mwaandaaji wa Mashindano ya Maisha Pluss hayo, Masoud Kipanya  kutaka kujua ukweli wa Ushiriki wa Nape kuwa mgeni Rasmi katika Mashindao hayo,

Masoud,alikiri kwa Nape kutoa Ahadi hiyo Miaka miwili iliyopita na Kushangaa kiongozi kubadilika kiasi hicho.
“Mimi nimefanya hivi makusudi kumtangaza kwenye Runinga ili Nchi nzima ione ubabaishaji wa Viongozi wetu katika ahadi.yeye alikuja Miaka miwili iliyopita na nyie mlikuwa Mashaidi Jinsi alivyokuwa anatoa Ahadi nashangaa leo anavyobadilika”alisema Masoud.


No comments: