Sunday, May 18, 2014

CHUO KIKUU CHA IRINGA WAZINDUA TAWI LA WANAFUNZI WANAOSOMA KISWAHILI AFRIKA MASHARIKI

chuo kikuu  cha Iringa
Mgeni  rasmi  akiandaliwa  shimo kwa ajili ya kupanda mti  mchawakama
Msanii  akitumbuiza  kwa  nyimbo
wanachama  wa  chawakama chuo cha Iringa
wanachama  wa  Chawakama  wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi
Mlezi  wa   CHAWAKAMA chuo  kikuu cha Iringa Bi Tulla Tweve akitoa maelezo  wa  chama  hicho

Mgeni  rasimi katika uzinduzi  wa tawi la wanafunzi  vyuo  vikuu  wanachama  wa chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAWAKAMA)afisa utamaduni mkoa wa Iringa Kenneth Komba  wa tano  waliosimama kutoka kushoto akiwa na wanachama wa  chama hicho tawi la chuo  kikuu cha Iringa mara baada ya kuzindua tawi hilo
………………………………………………………………………..
Na Mwandishiwetu blog
WANAFUNZI wa  chuo  kikuu cha  Iringa zamani Tumaini  wamewataka  wajumbe  wa  bunge  la katiba  kuhakikisha  wanapigania  lugha ya Kiswahili  ili  iweze  kupewa nafasi kubwa katika katiba mpya.
Rai   hiyo  imetolewa   na mlezi  wa wanafunzi  wa chama  cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAWAKAMA) Tullah Tweve  wakati  wa  uzinduzi  wa tawi  hilo chuoni hapo  jana 
Tweve  alisema  kuwa hakuna faida  kubwa  kwa taifa  kama kutumia  lugha  ya Kiswahili kama lugha  kuu katika taifa na hata  kuitumia katika kufundishia mashuleni na vyuo. 
Alisema  wakati  huu ni  wakati  mzuri  wa Taifa  kuweza  kurekebisha makosa  yaliyokuwepo katika kuchanganya lugha na kukumbatia  lugha  za mataifa  mengine na  kuacha  lugha  yetu . 
Hata   hivyo  alisema  kuwa yeye kama mwalimu  wa  Kiswahili katika  chuo  hicho moja kati ya mambo ambayo anayapa  kipaumbele ni pamoja na kiswahili kupewa kipaumbele. 
Kwa  upande  wao  wanafunzi  wanachama  wa  Chawakama  walisema  kuwa  walengwa  wakuu  wa chama  hicho ni  wanafunzi wa  vyuo  vikuu  wanaosoma  Kiswahili na kuwa  wanachama ni nchi  tano barani Afrika kama Tanzania ,Uganda , Kenya ,Rwanda  na Burundi lea  kusihiriki makondamano mbali mbali barani Afrika . 
Pia walisema  kuwa msukumo wa kuanzisha  Tawi hilo ulitokana na jitihada za mwalimu Tulla Tweve na  Albart Chalamila na kuwa  tawi  kwa  sasa  linawachama  zaidi ya 60. 
Walisema  kuwa  chama hicho kimeanzishwa  mwaka 2002  na  kuwa katika chuo  cha  Iringa tawi  hilo  lilianzishwa mwaka 2010 na  kuwa mbali ya kutokuwepo kwa  tawi  ila bado  wanafunzi  wa  somo la kiswahili  waliende 
Aidha  walisema  changamoto  kubwa ni  kukosekana kwa  fedha  za  kuendeshea chama pamoja na chama hicho  kutotambulika kwa  kuwa na uongozi  wa unaojulikana na chuo  hicho. 
Afisa  utamaduni mkoa wa  Iringa Keneth Komba mbali ya  kuwashukuru  wanachama wa  chama  hicho  cha Chawakama kwa kuenzi  kiswahili bado alisema  kuwa jitihada  hizo  kubwa  zilizoanzishwa na chuo hicho. 
Hata  hivyo alisema  kuwa  wenye  uwezo  wa  kukuza  kiswahili ama  kubomoa  lugha ya kiswahili ni  wasomi wenyewe ambao  wamepelekea  kuyumbisha  lugha . 
Komba  alisema  kuwa  mikataba mibovu ya  kifisadi katika Taifa  inasababishwa na lugha ya kiingereza ambayo wengi  wa 
“Tunatambua  kuwa  duniani  kuna  lugha  zaidi ya  16 ikiwemo  lugha ya  kiingereza ,kifaransa kirusi  na kiarabu na lugha  mbali mbali huku katika afrika lugha kuu ni kiswahili ambao lugha hiyo  imekuwa  ikiendelea  kukua  zaidi barani afrika “

No comments: