Thursday, May 22, 2014

MBEYA CITY YAENDA SUDAN

Timu ya Mbeya City inaondoka leo usiku (Mei 22 mwaka huu) kwenda Sudan kushiriki michuano ya Kombe la Nile Basin inayoanza kutimua vumbi kesho (Mei 23 mwaka huu) jijini Khartoum, Sudan.

Kikosi cha Mbeya City chenye watu 25 wakiwemo wachezaji 20 kinaondoka saa 2.55 usiku kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Nairobi ambapo kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 asubuhi kitaunganisha ndege nyingine hadi Khartoum.

Msafara huo wa kikosi hicho ambao utawasili Khartoum saa 7.30 mchana kwa saa za huko unatarajia kurejea nyumbani Juni 5 mwaka huu iwapo timu hiyo itafanikiwa hatua ya mwisho ya mashindano hayo.

Michuano ya Nile Basin imeanzishwa mwaka huu na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), na inashirikisha timu zilizoshika nafasi za pili katika ligi za nchi wanachama wa baraza hilo.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

No comments: