Tuesday, May 27, 2014

SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI--KITAIFA NI MWANZA,WAZIRI MAHENGE ATOA NENO

Watanzania wametakiwa kuungana kwa pamoja katika kuadhimisha siku ya mazingira duniani ambayo itaadhimishwa tarehe 5 mwezi juni mwaka huu ambapo kidunia siku hiyo itaadhimishwa katika kisiwa cha BARBADOS moja ya visiwa vya karibian na tanzania siku hiyo itaadhimishwa mkoani mwanza.

    Akitangaza maadhimisho hayo leo mbele ya wanahabari jijini dar es salaam waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira mh BINILIUS MAHENGE  amesema kuwa siku ya mazingira duniani iliamuliwa na azimio la baraza la umoja wa mataifa la mwaka 1972 kama kielelezo cha ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa umoja wa mataifa kuhusu mazingira uliofanyika huko stockholm nchini sweden.


        Waziri mahenge amekiri mbele ya wanahabari kuwa pamoja na siku hiyo kuadhimishwa kila mara hapa nchini lakini bado maeneo mengi ya majiji hapa tanzania ni machafu sana huku akitolea mfano jiji la dar es salaam ambapo limekuwa likiwa chafu kadiri siku zinavyozidi kwenda jambo ambalo amekiri kuwa bado ni changamoto kubwa kwake na kwa ofisi yake.


         Aidhia ametoa wito kwa watanzania wote kuadhimisha siku hiyo ya mazingira duniani kwa vitendo kwa kuhakikisha kuwa wanafanya usafi katika maeneo yao pamoja na kushirikiana na viongozi wao katika kufanya maeneo yao kuwa masafi  

No comments: