Monday, May 12, 2014

TIGO YAZINDUA SMARTPHONE APP YA KWANZA AFRICA MASHARIKI YA KUTUMA NA KUPOKEA PESA

Mkuu wa husuma za kifedha kutoka tigo ANDREW  HODGSON akizungumzia huduma hiyo mpya leo katika makao makuu ya tigo tanzania

          Kampuni ya simu za mkononi ya tigo Tanzania leo imezindua huduma mpya  ya kutuma na kupokea  pesa ambayo ni ya kwanza Africa ya mashariki itakayowezesha watumiaji wa simu  za aina ya ANDROID NA IOS nchini kutuma na kupokea fedha kwa njia rahisi na kwa ufanisi zaidi.

          Akizungumza na wanahabari leo makao makuu ya tigo mkuu wa huduma za kifedha ANDREW  HODGSON amesema kuwa kuanzia sasa watumiaji wa simu za kisasa SMARTPHONES nchini wataweza kufanya miamala yote ya tigo pesa kama kulipia huduma zote ,kulipa fedha benk,na kuongeza salio kwa haraka na urahisi zaidi kwa kutumia tigo pesa application.

Wanahabari wakisikiliza kwa makini leo


Amesema kuwa kuanzia sasa wateja wa tigo wanaweza kupata huduma zote za tigo pesa katika mtandao wa tigo bila kuingia gharama yoyote ya data,wateja pia watakuwa na uwezo wa kutumia account zao za tigo pesa popote pale walipo duniani kupitia internent ya wi-fi au mtandao wowote uliopo wa internent kupitia simu ili mradi awe amesajiliwa na tigo pesa.
 
        HODGSON  amesema kuwa kupata huduma hii mpya ya tigo lazima uwe na simu ya kisasa yani smartphone ambayo inatumia program ya IOS au ANDROID.

No comments: