Wednesday, June 11, 2014

BREAKING NEWZZ---YAMETIMIA TENAA---WAMBURA NOMA SASA RASMI--CHEKI HAPA

Mkutano unaondelea hapa TFF wa kumrudisha wambura kugombea uchaguzi wa simba
Kamati ya rufaa ya TFF muda huu imetangaza rasmi kumrejesha katika kinyanganyiro cha kugombea urais wa timu ya simba Tanzania aliyekuwa mgombea bw MICHAEL WAMBURA baada ya kumaliza kusikiliza rufaa yake na kubaini kuwa wambura bado anastahili kugombea urais katika timu hiyo

Kwa mujibu wa kamati hiyo ya TFF imesema kuwa Bw WAMBURA ni kweli alifungiwa na timu ya simba baada ya kuipeleka mahakamani lakini adhabu hiyo haikutekelezwa na kumfanya wambura aendelee kufanya kazi mbalimbali katika timu hiyo ikiwemo kushiriki katika kuunda kamati hiyo ya uchaguzi pamoja na kutengeneza katiba mpya.

---habari zaidi zitakujia-----

No comments: