Tuesday, June 24, 2014

HOT NEWZZ--POLISI KANDA MAALUM YATANGAZA MSAKO MKALI KUWAKAMATA MAJAMBAZI WALIOHUSIKA NA MAUAJI YA MTAWA (SISTA) PAMOJA NA MATUKIO MENGINE.


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limetangaza msako mkali wa kuwatafuta na kisha kuwakamata wale wote waliohusika katika tukio la kuuawa kwa kupigwa risasi kwa MTAWA wa Kanisa Katoliki Sista CRESENCIA D/O KAPURI, miaka 50, mhasibu Parokia ya Kanisa Katoriki Makoka,  lililotokea tarehe 23/06/2014 eneo la Ubungo Kibangu.

      Awali, marehemu akiwa ameongozana na wenzake ambao ni Sista BRIGITA D/O MBAGA, Miaka 32, Mkazi wa Makoka pamoja na dereva wao MARK S/O PATRICK MWARABU akiendesha gari aina ya T/Hilux PICK-UP namba T213 CJZ wakitokea benki ya CRDB tawi la Mlimani City, walipofika eneo la Ubungo Kibangu ili kulipa deni la chakula katika duka la bwana THOMAS S/O FRANCIS ndipo walipotokea majambazi wawili wakiwa na pikipiki ambayo haikusomeka namba na mmoja akiwa na bunduki aina ya SMG wakampiga risasi ya kidole gumba cha mkono wa kulia dereva wa gari hilo kisha kupiga mtawa huyo risasi ya kifuani na kupora mkoba uliokuwa na pesa kiasi cha Tshs: 20,000,000/= (million ishirini) na nyaraka mbalimbali za ofisi.


     Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi limeazimia kufanya yafuatayo:
·       Kwanza limegundua kwamba matukio ya ujambazi hasa unaohusian na wananchi kuporwa kiasi kikubwa cha pesa unaanzia katika mabenki ambapo majambazi huwafuatilia wateja waingiapo au kutoka katika benki mbalimbali.

·           Imeonekana kwamba mara nyingi mabenki yanapohitahi kusafirisha pesa nyingi hutumia escort ama ya Polisi au taasisi nyingine zinazotoa huduma ya ulinzi.

·                Ni muhimu kwa mabenki kuwahimiza wateja wao kutochukua kiasi kikubwa cha pesa kiholela kwani ni rahisi kuporwa na watu wasio na nia njema

·       Aidha mabenki yawahimize wateja wake kutumia njia mbadala za kusafirisha pesa nyingi kama vile matumizi “CHEQUE”, Kufanya miamala bila kadi (Cardless transactions), matumizi ya kadi za ATM, na njia nyinginezo za kifedha.   

·       Jeshi la Polisi linawahimiza mameneja wa benki zote kutoa taarifa polisi endapo kuna mteja yeyote atakaidi ushauri wa taasisi za fedha. Aidha benki ziwe na kitego


      Pia, tunawaomba wananchi watoe ushirikiano wa kutosha kwa jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za kutosha ili kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa wa ujambazi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake. Pia wafanyabiashara na taasisi nao na wasitumie njia za mkato kwa faida ya ulinzi wa maisha na mali zao. Aidha, benki ziwe na kitengo cha ushauri wa usalama wa wateja. Ni muhimu watumie mitandao ya usafirishaji fedha ambayo ni salama kama vile M-PESA, AIRTEL Money, TIGO Pesa, Easy Pesa, nk.

No comments: