Saturday, June 28, 2014

TIGO YAWEZESHA MAFUNZO YA TECHNOHAMA KWA WASICHANA JIJINI DAR ES SALAAM

Badhi ya wasichana kutoka shule mbalimbali jijini dar es salaam wakiwa katika mafunzo hayo
 Wasichana nchini Tanzania wamepewa changamoto ya kujiendeleza katika masomo ya technohama ili kuweza kuongeza upeo wao katika matumizi ya computer na kuweza kuchangia katika maendeleo ya kijamii kwa ujumla nchini Tanzania.
 Changamoto hiyo  imetolewa leo jijini Dar es salaam na meneja wa uwajibikaji kwa jamii kutoka kampuni ya tigo Tanzania Bi WOINDE SHISAEL wakati akizungumza na wanafunzi wa kike wapatao 100 kutoka shule za secondary mbalimbali waliokuwa katika mafunzo maalum ya technohama  yaliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali linalijihusisha na technohama APPS AND GIRLS ambao pia ni mmoja wa washindi wa program maalum ya wajasiriamali wa kijamii TIGO REACH  FOR CHANGE
 Bi WOINDE amesema kuwa “mkakati wa huduma ya uwajibikaji walionao tigo ni kuwezesha jamii kupitia matumizi ya vyombo vya kidigital” ambapo ametoa rai kwa wanawake na wasichana wote kujitokeza zaidi kujiendeleza kidigital kupitia technohama huku akiongeza kuwa ni dhana potofu kuwa wasichana hawawezi kufanya vizuri katika technohama wakati wana nafasi kubwa sana.
Aidha amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga wasichana tu kwa sababu wanawake wengi wameonekana kuwa nyuma sana katika kujihusisha katika technohama.
 Meneja wa uwajibikaji kwa jamii kutoka kampuni ya tigo Tanzania Bi WOINDE SHISAEL
Muasisi wa APPS AND GIRLS bi CAROLYNE  EKYARISIIMA
Naye muasisi wa APPS AND GIRLS bi CAROLYNE  EKYARISIIMA ampaye pia ni mmoja wa washindi wa dola 25,000 za kimarekani kutoka tigo reach for change kwa mwaka huu amesema kuwa mafunzo haya yanazingatia kwapatia wasichana utaalam katika kutengeneza tovuti kama njia moja wapo ya kuwahamasisha katika maswala ya technohama.

Shule zilizohudhuria mafunzo hayo ni pamoja na kisutu,jangwani,na kibasila ambapo mafunzo hayo ni ya simku moja.

No comments: