Monday, June 16, 2014

TOFAUTI KATI YA BAJETI YA SERIKALI NA BAJETI MBADALA YA KAMBI RASMI YA UPINZANI KWA MWAKA 2014/2015.



BAJETI MBADALA YA KAMBI YA UPINZANI 2014/2015
BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA 2014/2015
1
Bajeti isiyo na Mikopo ya kibiashara hivyo bajeti inalenga kulipunguzia taifa mzigo wa madeni.
Bajeti ya Serikali ina mikopo yenye masharti ya kibiashara ya shilingi trilioni 4.3 na hivyo bajeti hii inawaongezea wananchi mzigo wa madeni.
2
Bajeti inayoendelea kusisitiza umuhimu wa kuwalipa pensheni wazee wote nchini wenye umri wa   miaka 60 na kuendelea.

Bajeti ya Serikali iko kimya kabisa kuhusu malipo ya pensheni kwa wazee wote nchini.
3
Bajeti inayoendelea kusisitiza kushusha kiwango cha  tozo ya kodi ya mapato ya ajira kwa wafanyakazi (PAYE) hadi kufikia asilimia 9.
Bajeti ya Serikali imeendelea kuwakandamiza wafanyakazi kwa kutoza asilimia 12 ya  kodi ya mapato ya ajira (PAYE)  kwa wafanyakazi.
4
Bajeti ya Upinzani imeainisha vyanzo vipya  vya mapato ya ndani na hivyo  inayojitegemea kwa asilimia 84.38
Bajeti ya Serikali ni  tegemezi kwa asilimia 36.4 kutokana na kukopa kwa kiwango kikubwa na hivyo  kuongeza deni la taifa.
5
Bajeti Mbadala, mapato ya ndani ni asilimia 34.55 ya pato la Taifa
Bajeti ya Serikali, mapato ya ndani ni asilimia 23 ya pato la taifa.
6
Bajeti inayolenga kupunguza misamaha ya Kodi hadi kufikia asilimia 1 ya Pato la Taifa ili kuongeza mapato ya ndani.
Bajeti ya Serikali imetaja tu azma ya kupunguza misamaha ya kodi lakini haijataja ni kwa asilimia ngapi ya pato la taifa wala haijaainisha watakaofutiwa misamaha hiyo.
7
Bajeti inayolenga kutekeleza kikamilifu  miradi ya maendeleo kwa kutenga asilimia 42.67 ya bajeti yote kugharamia miradi ya maendeleo.
Asilimia 22 ya Bajeti yote ya  Serikali inakwenda kulipa deni la Taifa na asilimia 67.5 ni  matumizi ya kawaida. Hivyo miradi ya maendeleo haijapewa kipaumbele.
8
Bajeti inayolenga kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo ambavyo havimuumizi mwananchi wa kawaida
Bajeti ya Serikali imelenga kukusanya mapato kutoka katika bidhaa zinazotumiwa kila siku na wananchi kama vile vinywaji na hivyo kuwaongezea wananchi ugumu wa maisha.
9
Matumizi ya Kawaida ni asilimia 57.33 tu ya bajeti yote
Matumizi ya Kawaida ni  67.5%
10
Bajeti ya kumsaidia mwananchi wa kawaida kutoka katika wimbi la umaskini.
Bajeti isiyo mtambua mwananchi maskini na kuongeza matumizi makubwa kwa watawala.






No comments: