Na optatucy stan
Jukwaa
la katiba Tanzania JUKATA leo limewasihi wajumbe wa bunge la katiba wanaounda
umoja wa katiba ya wananchi UKAWA kurejea katika bunge linalotarajiwa kuanza
mapema mwezi kesho kwa kwa masharti ya kufwata rasimu ya katiba mpya
iliyopelekwa bungeni na tume ya mabadiliko ya katiba Tanzania.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es salaam
mwenyekiti wa jukwaa hilo DEUS KIBAMBA amesema kuwa JUKATA walifanya utafiti chini ya jopo maalum na
kupata nafasi ya kuzungmza na makundi mbalimbali ya wananchi ambao wengi wao
waliwataka UKAWA kurejea bungeni kutokana na umuhimu wa bunge hilo kwa
watanzania.
Bw KIBAMBA amesema kuwa jopo hilo limepata nafasi ya
kuzungumza na wadau mbalimbali wa kisiasa,asasi za kiserikali na zisizo za
kiserikali ambapo amesema kuwa mengi ya ,makundi hayo yameeleza kuwa kutokana
na maslahi ya bunge hilo kwa watanzania kuwa ni makubwa sana wabunge
wanaowakilishja umoja wa UKAWA wanapaswa kurudi bungeni ila kwa masharti ya
kuendelea na majadiliano ya rasimu ya katiba mpya na si vinginevyo.
Aidha KIBAMBA ameeleza kuwa mchakato wa uundwaji wa
katiba mpya ni jambo la muda mrefu na linahitaji busara ya kutosha hivyo amemtaka
spika wa bunge hilo Bw SAMWELI SITTA kuwa kinara wa kutatua tofauti
zinapojitokeza kwenye bunge hilo miongoni mwa wabunge.
Kwa upande wake mkuu wa shule ya sheria ya chuo kikuu cha kenyeta cha nchini kenya Bw PATRICK LUMUMBA amemsihi rais wa Tanzania JAKAYA KIKWETE kuwa na busara katika kipindi hiki cha mabadiliko ya katiba huku akisisitiza kuwa Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa mataifa mbalimbali hivyo inatakiwa kuonyesha democrasia ya kweli katika mchakato huu,
huku akiwasihi watanzania kuutumia mchakato huu kupata katiba mpya ili kuepuka machafuko kama baadhi ya mataifa ya africa kwa sasa
No comments:
Post a Comment