Wednesday, July 23, 2014

SIMULIZI ZAIDI JUU YA MKASA WA KUFUNGIWA GAZETI LA MWANAHALISI


Na karoli Vinsent

            BADO mtandao huu unaendelea na Simulizi endelevu Juu ya kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi,ambapo mtandao huu unafanya hivi ili kwenda sawa na Tarehe ambayo gazeti hili lilifungiwa na Serikali kwa mda usiojulikana,Gazeti la mwanahalisi ifikapo tarehe 25 mwezi wa saba mwaka huu linatimiza Miaka miwili tangu lifungiwe na serikali.

 Ambapo Gazeti hili lilifungiwa rasmi tarehe 25 mwezi wa 7 mwaka 2012,kutokana na kuandika habari zinazodaiwa ni za kichochozi,

       Leo ni siku ya tatu ambapo bado mtandao huu,unazidi kuendelea na simulizi hiyo,ambapo Jana tuliiweka habari iliyopeleka kufungiwa kwa Gazeti hilo,Habari yenyewe ilikuwa inamzungumzia Sakata nzima la linalomuhusu mwenyekiti wa Chama cha Madaktari nchini Dk Stevin Ulimboka ambaye Gazeti hilo liandika juu ya mtu waliombaini kwamba anahusika kumfanyia unyama Dokta huyo.


               Baada ya kuandika habari hiyo kwenye toleo namba 304,likamfanya Waziri wa Habari,utamaduni na Michezo kulifungia Gazeti hilo,katika Tamko lake kwenye Vyombo vya Habari,ambapo alisema amelifungia Gazeti hilo kwa mda usiojulikana na kusema Gazeti hilo limekuwa likiandika Habari za Uchochezi pamoja kuleta Uhasama kati ya vyombo vya Dola pamoja na wananchi,

        Katika Tamko hilo lilosainiwa na msajili wa Magazeti nchini,alisema kutokana na Sheria ya magazeti ya Mwaka 197o kifungu cha 25,ambacho kimempa mamlaka ya kulifungia Gazeti,

       Ambapo alizidi kusema Mhariri wa Gazeti hilo ameitwa mala kwa mala na Wizara yake ili aweze kutoa Ushahidi au kutoa ufafanuzi juu ya anachokiandika na Mhariri huyo alijitetea na kusema katiba ya Nchi ibara ya 18 inampa mamlaka kutoa maoni.

          Usikose tena kuendelea kusoma mwendelezo wa Makala hizo zinazozungumzia kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi,amabapo uchambuzi huu umekuja ikiwa ikenzi miaka miwili Tangu gazeti hilo la mwanahalisi ,ambapo gazeti hilo,Tarehe 25 mwezi huu linatimiza miaki miwili,

         Na kesho mtandao huu utakuja na Jinsi wanasiasa pamoja na Wanaharakati walipoibuka na kupingana na Adhabu hiyo iliyotolewa kwa gazeti hilo  

No comments: