SIKU moja
kupita Baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema kusema uwezekano wa kupata katiba mpya haupo, kutokana na Bunge la Katiba kukosekana Theluthi 2 ya wajumbe kutoka
Zanzibar,kukosekana huko kunatokana na Wajumbe wanaounda Umoja wa Kutetea
Katiba ya Wananchi UKAWA kugoma kurejea kwenye Bunge hilo.
Nao Umoja wa Kutetea Katiba ya
Wananchi UKAWA,Umeibuka na kumvaa Mwanasheria wa Serikali Jaji Fredrick Werema
na kusema kama anajua katiba haipatikani kuna ulazima gani wa kutumia Mabilioni
ya Watanzania kwenye Bunge hilo, wakati Fedha
hizo zingeenda kwenye masuala mengine ya Maendeleo ikiwemo kwenye kuboresha
Daftari la Kudumu la wapiga kura.
Kauli hiyo imetolewa Leo Jijini Dar
Es Salaam na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi James Mbatia wakati alipokuwa
anaongea na Waandishi wa Habari,ambapo Mbatia alisema anamshangaa sana
Mwanasheria Mkuu wa Serikali kujua huwezekano wa kupata katiba mpya haupo ,kwanini anashindwa kumshauri Rais
Jakaya Kikwete kulivunja Bunge hilo la Pesa kulekezea kwenye kwenye mambo
mengine.
“Nashangaa sana kwa huyo
mwanasheria wa serikali anajua kabisa katiba haipatikana kwasababu ya Bunge
hili kukosa Theluthi 2 ya wajumbe ambao wengi wao ndio sisi UKAWA ambao
tumegoma kurejea kwenye bunge hilo kutokana na hujuma,ni bora tu Bunge hili
livunjwe kwasababu katika haitopatikana kwa hali hii ilivyo,sasa yeye anasema
bunge liendee,litaendelea vipi wakati anajua katiba haipatikani?”alihoji
Mbatia.
Mbatia ambaye naye pia ni Mjumbe wa
Bunge Maalum la Katiba alizidi kusema Mchakato wa katiba unaoendelea sasa
katika Bunge Maalum la Katiba haujalenga kusimamia Maslahi mapana ya Watanzania
kwa ujumla,bali umeporwa na kikundi cha watu wachache wnaotaka kutimiza malengo
yao Binafsi hasa
kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Aidha,James Mbatia ambaye pia
ni Mbunge wa kuteuliwa na Rais,alisema kwa hali ilivyo sasa ni Vema Bunge
maalum la Katiba liharishwe mpaka pale muhafaka wa Kimataifa utakapopatikana
kwa njia ya Maridhiano.
Vilevile Chama cha NCCR mageuzi
kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC iweke hadharani daftari la kudumu la
wapiga kura liloboreshwa mwaka 2010 kwa kutumia mabilioni ya shiringi ya Watanzania,kwa
kuwa chama hicho kimeshtushwa na taarifa za Tume kusema hakuna daftari wapiga
kura.
Pia chama hicho kimezidi
kushikilia msimamo wake wakutorejea kwenye Bunge hilo maalum la Katiba kwa
madai mchakato huo wa katiba kuingiliwa na chama cha mapinduzi,na kusema
Wajumbe waote wa Bunge maalum la Katiba wanaotokana na chama hicho,
kutoshiriki katika vikao hivyo vinavyoendelea
hadi madai ya msingi ya chama hicho pamoja washiriki wake ambao ni Vyama vya
Chadema,CUF,DP na NLD yatakapopatiwa Ufumbuzi.
Kauli hiyo ya Mbatia inazidi inazidi
kuwachanganya Watanzania kutokana na Viongozi wa Serikali ya Rais Jakaya
Kikwete kuzidi kujichanganya kutokana hoja ya theluthi 2 ya wajumbe.
Ambapo ikulu ya Kikwete katika
tamko lake lilosainiwa na Kur
ugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilisema Katiba Mpya
itapatikana bila ya kuwepo UKAWA,kwani Theluthi 2 ya wajumbe inapatikana kwenye
Bunge hilo.
Na kuzidi kusema Umoja wa huo wa Ukawa ni
Idadi ndogo sana,Kauli hiyo ya ukakasi ya Ikulu iliwai kutolewa na Mwenyekiti
wa Bunge Maalum la katiba Samwel Sitta ,
Baada ya Ikulu kutoa kauli hiyo,ndipo
Jana Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema aliibuka na kupingana na
Ikulu na kusema uwezekano wa kupata katiba mpya haupo, kutokana na Bunge hilo
kukosa idadi ya Theluthi 2 ya wajumbe,na kusema endapo ikishindikana itabidi
Bunge hilo lisimame na kutoa mwanya kwa Bunge la kawaida liifanyie marekebisho
katiba iliyopo hususani kipengere cha tume ya uchaguzi na vingine,ili baada
mchakato huu uendelee kama kawaida baada ya kumalizika uchaguzi Mkuu.
“Kuhusu Idadi ya kura za wajumbe
wabunge maalum la katiba inatoa wasiwasi kwasababu kwenye Kamati zile theluthi
2 ya wajumbe inapatikana bila shida ila tatizo itakuja wakati wakupitisha
Rasimu iliyojadiliwa na Bunge ndio itatupa shinda kwasababu lazima ipatikane
theruthi ya 2 ya wajumbe wa Tanzania Bara na,”
“ Zanzibar sasa ungiangalia hapa kwa hali ilivyo kama ikiendelea hivi bila ya kuwepo UKAWA itakuwa ni shida kupata Theluthi 2 ya awajumbe wa Zanzibar na hapa ndio watu wanasema tutakuwa tumetumia pesa nyingi sana za walipa kodi harafu hakuna katiba ndio maana nawaomba ukawa warejee”alisema Werema
No comments:
Post a Comment