Mkurugenzi wa kampeni wa CHADEMA SINGO BENSON akitangaza matokeo ya uchaguzi huo muda huu jijini Dar es salaam |
Chama cha
Democrasia na maendeleo chadema muda huu kimetangaza matokeo ya uchaguzi wake
wa kwanza wa chaguzi zake za ndani ya chama ambapo kwa safari hii ni uchaguzi
wa baraza la wazee la chama hicho uchaguzi uliofanyika juzi tarehe 6 jijini dare s salaam na kumalizika usiku.
Akizungumza na wanahabarai muda huu makao makuu ya
chama hichi konondoni jijini dare s salaam mkurugenzi wa kampeni wa chama hicho
SINGO BENSON KIGAIRA amesema kuwa uchaguzi huo ulimalizika kwa amani na baraza
hilo kupata viongozi wake wapya ambao watadumi katika nafasi hizo kwa muda wa
miaka mitano kuanzia sasa.
Mwenyekiti mpya wa baraza la wazee la CHADEMA mzee HASHIM JUMA ISSA akitambulishwa mbele ya wanahabari muda huu baada ya kuibuka mshindi katia uchaguzi huo |
Akitaja majina ya wagombea nafasi ya mwenyekiti wa
taifa wa baraza hilo la wazee ameshinda mzee HASHIM JUMA ISSA kutoka Zanzibar ambaye
ametangazwa rasmi kuwa mwenyekiti mpya wa baraza hilo la wazee la CHADEMA
taifa.
Nafasi ya makamu mwenyekiti wa baraza hilo la wazee
kwa upande wa bara imechukiliwa na mh SUZAN LYIMO ambaye sasa ametengazwa rasmi
kuchukua nafasi hiyo,huku nafasi ya makamu mweyekiti wa baraza hilo kutoka zanzibari
ikichukuliwa na mzee OMAR MASOUD OMAR.
MH SUZAN LYIMO ambaye kwa sasa ni makamu mwenyekiti bara akitambulishwa pia |
Katika nafasi ya katibu mkuu wa baraza hilo la wazee
la chama hicho aliyeshinda ni mzee RODRICK EMMANUEL LUTEMBEKA ,huku nafasi ya
mwekahazina wa baraza hilo ikichukuliwa na ERASTO SINGIRA GWOTA .
Aidha katika nafasi ya ujumbe wa baraza kuu taifa
KUTOKA BARA walioshinda ni ALFRED
NTUPWA,FLORENCE KASILIMA,HUGO KIMARYO, pamoja na VICTOR KIMESERA.huku nafasi ya
ujumbe wa baraza kuu kutoka Zanzibar ikichukuliwa na HASHIM JUMA ISSA pekee
baada ya wajumbe wengine wawili kujitoa kabla ya uchaguzi huo.
Nafasi nyingine iliyokuwa inahitajika ni nafasi ya
wajumbe wa mkutano mkuu kutoka bara ambapo waliochaguliwa ni CHARLES
KIKOMINGO,MARY NAKOE,MARRY JOACHIM,SYLIVESTER SHIRIMA,TIMOTH KIRWAY,pamoja na
WILLIAM MWANGWA huku kutoka Zanzibar wakiwa
ni HASSAN KHERI,KHATIBU ALLY KHATIBU,HAJI KALI HAJI,pamoja na RABIA,OMAR
No comments:
Post a Comment