Tuesday, September 30, 2014

TIGO WASHIRIKI KIKAMILIFU KUSAIDIA KUINUA SOMO LA HESABU KWA WANAFUNZI WA TANZANIA

Mkurugenzi wa tigo tanzania DIEGO GUTIEREZ akizungyumza katika hafa iliyoandaliwa na MICROSOFT pamoja na NOKIA kwa kushirikiana na wizara ya mawasiliano sayans na technologia ambapo tigo nao wamechangia kwa kiasi kikubwa katika kutimiza malengo ya huduma hiyo mpya iliyozinduliwa.
  Wanafunzi nchini wametakiwa kuhakikisha kuwa wanatumia vifaa vya electronic mfano computer na simu za mkononi  kama njia moja wapo ya kujifunzia na kupata elimu badala ya kutumia kwa nzia zisizofaa.


Wito huo leo umetolewa na mkurugenzi wa kampuni ya mawasiliano ya tigo Tanzania DIEGO GUTIEREZ wakati akizungumza katika hafla iliyoandaliwa na MICROSOFTna NOKIA  kwa kushirikiana na wizara ya mawasiliano sayansi na technologia ya uzinduzi wa  (NOKIA MOBILE MATHEMATICS FOR TANZANIA),kupata masomo ya sayans hususani somo la hesabu kwa njia ya simu za mkononi na vifaa vingine.

Mkurugenzai huyo amesema kuwa kuna dhana potofu iliyojengeka kuwa masomo ya sayansi hususani somo la hesabu ni masomo magumu yasiyowezekana jambo ambalo amesema kuwa sio kweli kwani kwa matumizi wa vifaa na huduma hiyo masomo hayo yatakuwa masomo pendwa kwa wanafunzi wa Tanzania.

Huduma ya NOKIA MOBILE MATHEMATICS FOR TANZANIA iliyozinduliwa leo ni huduma inayowawezesha wanafunzi kupata masomo kwa njia za eleconic ambapo huduma hii ilianzia nchini Africa kisini mwaka 2008 na Tanzania kuwa nchi ya pili kupata huduma hii, ambapo baada ya utafiti kuonyesha kuwa wanafunzi wanapenda sana matumizi ya simu ikaonekana huduma hii itawasaidia wanafunzi katika masomo hayo.

Katika hatua nyingine kampuni yaTIGO Tanzania imeahidi kutoa FREE DATA kwa wanafunzi wote watakao kuwa wanatumia huduma hii ya NOKIA MOBILE MATHEMATICS FOR TANZANIA.




No comments: